Skip to main content

MAMLAKA ZA UPIMAJI DODOMA KUENDELEA KUPIMA MAKAZI YA WANANCHI


Image result for KUPIMA MAKAZI JIJIJINI DODOMA







Mamlaka zinazohusika na zoezi la upimaji wa makazi katika jiji la Dodoma zimeombwa kuendelea kupima viwanja vya wananchi katika maeneo mbalimbali ya jiji ikiwemo kata ya Mkonze ili kuepusha ujenzi holela.

Wito huo umetolewa leo na mwenyekiti wa mipango miji na mazingira kutoka jiji la Dodoma ambaye pia ni diwani wa kata ya Mkonze  BW, David Bochela wakati akizungumza na DODOMA FM na kusema kuwa suala la kupima linapaswa kuzingatiwa ili kuendana na hadhi ya jiji.

Amesema kuwa nia ya wananchi ni kujenga ili waishi katika makazi bora hivyo viongozi mbalimbali ikwemo wa serikali za mitaa wana wajibu wa kusimamia jambo hilo kwani jamii bado inahitaji kupewa elimu ili kutokomeza suala la ujenzi holela ambalo limekuwa likikwamisha shughuli za maendeleo.

Hata hivyo amewataka wananchi kuunga mkono jitihada za viongozi pamoja na kuyapokea makampuni yanayohusika na suala la upimaji wa makazi pindi yanapofika katika maeneo yao ili kufanikiwa jambo hilo kwa wakati.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi jijini Dodoma wamesema kuwa ujenzi holela umekuwa ukichangiwa na gharama za upimaji kuwa juu ukilinganisha na vipato vyao hivyo ni vyema serikali ikatazama jambo hilo ili kufanikisha zoezi hilo.

NA ALFRED BULAHYA                                               DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...