Skip to main content

WAHITIMU CHUO CHA SERIKALI ZA MITAA HOMBOLO KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA AJIRA

                                           

Image result for uzinduzi wa mnara wa Magufuli Hombolo

SERiKALI kupitia wizara ya nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI imesema itahakikisha inatoa ajira za watendaji wa vijiji na kata kutoka katika chuo cha serikali za mitaa cha HOMBOLO kutokana na wahitimu hao kuwa na uwezo mkubwa wa kusimamia mambo mbalimbali katika jamii kupitia elimu wanayoipata.

Kauli hiyo imetolewa na waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Selemani Jafo wakati akizungumza katika uzinduzi wa mnara wa Magufuli (MAGUFULI SQUARE) uliojengwa katika chuo cha serikali za mitaa kilichopo kata ya Hombolo mkoani Dodoma.

Waziri Jafo amesema wanafunzi wanaotoka katika chuo hicho ndio hasa watakaokwenda kufanya kazi katika mamlaka za serikali za mitaa kutokana na wahitimu hao kukidhi vigezo vya kuwasimamia wananchi hivyo ni wajibu wa serikali kuwapatia ajira ili kuleta ufanisi katika kazi hasa katika wizara hiyo.

Aidha Jafo ameahidi kukisimamia chuo hicho ili kiweze kutoa wahitimu walio na uelewa mkubwa katika suala la usimamizi wa mambo mbalimbali ya kijamii ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kinatoa elimu kuanzia ngazi ya astashahada ,stashahada na shahada.

Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya udhamini wa chuo hicho prof Suleimani Ngwale amewataka wanafunzi wote wanaohitimu katika chuo hicho kutumia mnara huo kujipima na kuenzi matendo yanayofanywa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

Naye mkuu wa chuo hicho dokta Mpamila Madale ameahidi kuyatekeleza mambo muhimu yote yaliyoelekezwa na serikali ili kuendelea kuboresha chuo hicho.

Na Alfred Bulahya                                                      Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifugua kwa upasuaji na

YANGA KESHO KUJUA ANACHEZA NA NANI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

MAJINA ya vigogo wa soka Afrika, wakiwemo mabingwa wa Afrika 1998, Raja Casablanca yametawala katika orodha ya wapinzani wapya wa Yanga kwenye michuano ya Afrika. Yanga SC imeangukia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambako watamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo. Hiyo ni baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Township Rollers Jumamosi jioni Uwanja wa Taifa mjini Gaborone nchini Botswana. Matokeo hayo yanamaanisha Rollers inakwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza historia hiyo kwa ushindi wa jumla wa 2-1 uliotokana na matokeo ya mchezo wa                              kwanza Dar es Salaam Machi 6. Na Yanga SC itamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo, ambazo ni CR Belouizdad, USM Alger za Algeria, Al-Masry ya Misri, Djoliba ya Mali, Raja Casablanca, Enyimba ya Nigeria, SuperSport United ya Afrika K