Skip to main content

HOSPITALI YA BENJAMINI MKAPA KUTATULIWA CHANGAMOTO YA MADAKTARI BINGWA

                               Image result for hospitali ya Benjamin Mkapa

Serikali imesema inatambua changamoto ya upungufu wa madaktari bingwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Mkoani Dodoma huku mikakati mbalibali ikifanyika ili kutatua changamoto hiyo.

Naibu Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dokta Faustine Ndugulile ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Rukia Ahamed aliehoji Serikali ina mpango gani katika kutatua changamoto ya upungufu wa madaktari bingwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa.

Dokta Ndugulile amesema Serikali imeweka mikakati ya kuondoa changamoto hiyo katika hospitali ya Benjamin Mkapa pamoja na hospital nyingine za rufaa za Mikoa zilizo na upungufu wa madaktari pamoja na kufadhili masomo ya madaktari bingwa wapatao 125.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa TAMISEM Mh. Josephat Kandege amesema nia ya Serikali ni kuhakikisha kuwa vituo vya afya na zahanati zinatoa huduma stahiki kwa wananchi na kusisitiza kuwa popote itakapobainika kituo cha afya kufungwa kwa kukosa watumishi wa afya ni vema taarifa zikatolewa mapema ili kufanyia kazi changamoto hiyo.

Mh. Kandege amesema baadhi ya maeneo yatakayopatiwa kipaumbele cha kujengewa vituo vya afya ili kuepusha msongamano katika hospitali za Wilaya ni pamoja na mkoa wa Kigoma ikiwa ni mkakati unaotegemea bajeti pamoja na kibali cha ajira kwa waganga wapatao 1667.
Na Pius Jayunga                                           Chanzo: Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...