Skip to main content

WATU WANNE DODOMA WASHIKILIWA KWA KUJIFANYA MAAFISA WA JWTZ NA USALAMA WA TAIFA

         
                       


Jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu 14 kwa makosa mbalimbali wakiwemo wanne kati yao kwa kujifanya maafisa wa jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ na usalama wa Taifa huku wakitumia nyadhifa hizo kujipatia mali kwa njia za udanganyifu.

Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma Gilles Muroto akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amewataja waliokamatwa katika tukio hilo kuwa ni Shaban Ramadhan Kwiyela (58) mkazi wa Igunga Tabora, Emmanuel Kasunga ( 45) mkazi wa Mtera Iringa, Juma Almasi Pembambili (33) mkazi wa Sai jijini Mbeya pamoja na Emmanuel Hassan Mwangolela (50) mkazi wa mtaa wa Ghana jijini Mbeya.

Katika tukio la pili wamekamatwa watu wawili kwa kujihusisha na wizi wa pikipiki huku wakitumia mbinu ya kuiba pikipiki kutoka Dodoma na kwenda kuziuza Kiteto Manyara na nyingine wakiiba kutoka Kiteto na kuzileta kuziuza hapa Mkoani Dodoma.

Kamanda Muroto amesema tukio la tatu wamemkamata kijana Abdalah Hamza Salum (20) dreva wa bodaboda mkazi wa Area A Dodoma kwa kosa la unyang’anyi ambapo hutumia pikipiki yake yenye namba za usajiliu MC. 366 BJR aina ya boxer kukwapua mikoba ya wapita njia na akipakia abiria huwapeleka katika maficho na kuwatishia sime kisha kuwapora vitu mbalimbali zikiwemo simu za mkononi, mikufu na vito vya thamani.

Katika tukio la mwisho kamanda Muroto amesema wanawashikilia watu 6 akiwemo raia wa china kwa kosa la kuchezesha mchezo wa kamari bila kibali maalumu katika mkoa wa Dodoma na hivyo kuikosesha serikali mapato na katika matukio yote kamanda Muroto amesema mkoa wa Dodoma utaendelea kukabiliana na kila aina ya uhalifu utakaojitokeza katika mkoa wa dodoma.

NA PIUS JAYUNGA                                                             DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...