Mauaji ya mwanafunzi Tanzania: Polisi wawahoji maafisa wakuu wa Chadema
Maafisa wa polisi mjini Dar es Salaam wamewataka viongozi wakuu wa chama cha upinzani nchini humo Chadema kufika mbele yake ili kuhojiwa kutokana na kifo cha mwanafunzi wa chuo kikuu cha usafirishaji nchini humo Akwilina Akwiline.
Bi Akwiline alifariki baada ya kupigwa risasi kimakosa wakati wa maandamano ya viongozi wa chama hicho yaliotibuliwa na maafisa wa polisi siku ya Ijumaa.
Mauaji hayo kwa sasa ndio swala linalozungumziwa sana nchini Tanzania huku raia kupitia mitandao tofauti ya kijamii wakishutumu kisa hicho.
Chanzo Bbc Swahili
JAMII YAOMBWA KUSAIDIA WATOTO WANAOISHI KATIKA MZINGIRA MAGUMU
Jamii imeombwa kusaidia makundi yenye uhitaji mbalimbali katika jamii zao ikiwemo watoto wanoishi katika mazingira magumu na hatarishi.
Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Dodoma Fatma Toffic ameyasema hayo katika halfa ya kukabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi waliopo katika kituo cha safina street network zilizotolewa na taasisi ya Miriam supporting society .Aidha amesema jamii inapaswa kujitoa katika kusaidia watoto wanaishi katika mazingira hatarishi huku akiwataka wazazi kuepuka mifarakano ambayo ndio imekuwa chanzo cha kuwa na watoto wengi wa mitaani.
Awali mkurugenzi wa taasisi ya Miriam supporting society Miriam Nteko amesema watoto wanaoishi katika mazingira magumu wamekuwa wakipata changamoto kupata matibabu kutokana na kukosa bima za afya na hivyo kuwaomba wadau wa maendeleo kuunga mkono suala hilo kwa kuendelea kuwakatia bima watoto hao.
Baadhi ya watoto waliopata bima hizo katika kituo cha safina street network akiwemo Amani Abdala ameshukuru kwa kupata bima hiyo na kusema itamsaidia pale atakapo pata matatizo ya kiafya
Jumla ya watoto 142 wamekatika bima za afya za CHF na taasisi ya Miriam supporting society kwa kushirikia na watu waliguswa kuwasaidia watoto hao.
Wananchi mkoani Dodoma wametakiwa kutoa taarifa dawati la jinsia juu ya vitendo vya kikatili vinavyoendelea kufanyika mkoani hapa ili kusaidiwa kutatuliwa matatizo yanayowakumba.
Akizungumza na kituo hiki mkaguzi msaidizi wa polisi dawati la jinsia na watoto Bi.Teresia Mdendemi amesema kwa kipindi kilichopita hakukuwa na kesi nyingi ambazo zilikuwa zinawafikia tofauti na kipindi hiki ambapo elimu imekuwa ikitolewa kwa jamii.
Bi. Mdendemi ametaja baadhi ya matukio ya kikatili ambayo yanaongoza kufanywa mkoani Dodoma kuwa ni pamoja na ubakaji,kulawiti, utelekezaji wa familia pamoja na ndoa za utotoni.
Kutokana na Elimu inayoendelea kutolewa dhidi ya upigaji vita matukio ya ukatili wa kijinsi wananchi mkoani Dodoma wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiano dawati la jinsia kwa kufikisha malalamiko yao ili kubaini mwitikio wa
HALMASHAURI YA MANISPAA YA DODOMA KUAJIRI ASKARI MIGAMBO 30.
Na Dodoma fm
Kamati ya fedha na mipango katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kwa kauli moja imekubaliana kuajiri askari migambo wapatao 30 watakao gawanywa katika tarafa 4 za Manispaa ya Dodoma ili kudhibiti ujenzi holela.
Mkurugenzi wa Manispaa
ya Dodoma Bw. Godwin Kunambi amewaambia waandishi wa habari kuwa lengo la kuajiri
migambo hao ni kuhakikisha wanadhibiti ujenzi holela ambao umekuwa ukiendelea
katika mji wa Dodoma ambao ndio kitovu cha Nchi.
Miongoni mwa mambo
mengine ambayo uongozi wa Manispaa ya Dodoma unaendelea kuyafanyia kazi ni
pamoja na kukamilisha ujenzi wa soko katika eneo la Makole litakalotumika kwa
shughuli zote za wamachinga ili kupunguza kero pamoja na msongamano wa
wafanyabiashara hao katika eneo moja.
Hata hivyo licha ya
kuwahamishia wamachinga wote katika soko la Makole Mkurugenzi wa Manispaa ya
Dodoma amesema ulinzi mkali utaimarishwa
katika maeneo ya barabara ili kudhibiti uzalishaji wa wamachinga wengine ndani
ya mji wa Dodoma.
Baadhi ya
wafanyabiashara maarufu kama wamachinga katika manispaa ya Dodoma licha ya
kupongeza jitihada hizo wamesema hatua hiyo itawarudisha nyuma kiuchumi
kutokana na wao kufanya biashara kwa kufuata maeneo yaliyo na mkuanyiko mkubwa
wa watu.
VYOMBO VYA DOLA VYATAKIWA KUTUMIA BUSARA KATIKA UTATUZI WA MIGOGORO.
Na Dodoma fm
Vyombo vya Dola vimetakiwa kuwa kipaumbele kwa kutumia nafasi zao katika kudumisha amani ya nchi hasa katika maandamano na migomo inayotokea ili kuepusha nchi kuingia katika machafuko yanayoweza kujitokeza.
Vyombo vya Dola vimetakiwa kuwa kipaumbele kwa kutumia nafasi zao katika kudumisha amani ya nchi hasa katika maandamano na migomo inayotokea ili kuepusha nchi kuingia katika machafuko yanayoweza kujitokeza.
Hayo yameelezwa na
Mchambuzi wa maswala ya kisiasa Bw. Denis Nachipyangu wakati akizungumza na
Taswira ya habari ambapo amesema kuwa mara nyingi machafuko yanatokea iwapo
vyombo vya dola vikitumia nguvu katika kutatua migogoro au maandamano hivyo ni
vyema vikatumia akili na busara ili kuepuka kutokea kwa machafuko ya nchi.
Bw. Nachipyangu amesema
kuwa maandamano mengi yamekuwa yakipelekea machafuko kutokana na kuwa baadhi ya
watu wamekuwa na mawazo tofauti juu ya matokeo ya maandamano hayo ambapo wengi
wao wamekuwa wakihofia kutokea kwa vurugu na machafuko.
Sanjari na hayo Bw.
Nachipyangu ametoa rai kwa Wananchi
pamoja na vyombo vya dola kutokukiuka haki za kikatiba katika kufuata taratibu
na sheria za nchi badala yake vinatakiwa kutoa ulinzi kwa Wananchi ili waweze
kuendelea kuwa na imani na vyombo hivyo.
JAMII IMETAKIWA KUTUMIA VYOO VYA KISASA
Na Dodoma fm
Wakazi wa maeneo ya vijijini mkoani Dodoma wameshauriwa kuacha kuendelea kutumia vyoo vya zamani na badala yake wajenge vyoo vya kisasa vinavyosafishika kwa urahisi ikiwa ni njia mojawapo ya kujikinga na magonjwa ya kuambukiza.
Wakazi wa maeneo ya vijijini mkoani Dodoma wameshauriwa kuacha kuendelea kutumia vyoo vya zamani na badala yake wajenge vyoo vya kisasa vinavyosafishika kwa urahisi ikiwa ni njia mojawapo ya kujikinga na magonjwa ya kuambukiza.
Ushauri huo umetolewa na afisa afya wa
manispaa ya Dodoma Bwana Alek Saimon wakati akizungumza na kituo hiki ambapo
amesema katika maeneo ya vijijini bado wanajamii hawana elimu ya kutosha juu ya
ujenzi wa vyoo bora vya kisasa ambavyo ni rahisi kuvisafisha.
Bwana Alek amesema katika kuhakikisha
afya katika jamii inaendelea kuimarika manispaa ya Dodoma wanashirikiana na wadau mbalimbali katika ujenzi wa vyoo bora na
vya kisasa kwa gharama nafuu pamoja na utoaji wa elimu zitokanazo na matumizi
ya vyoo hivyo.
Hata hivyo amesema maeneo mengi vijijini
wanashirikiana na ngazi ya kata ambao ni
maafisa afya wa kata wanao pita kila nyumba kuhamasisha wananchi juu ya ujenzi
wa vyoo bora na vya kisasa.
Comments
Post a Comment