Jamii imeombwa kusaidia makundi yenye uhitaji mbalimbali katika jamii zao ikiwemo watoto wanoishi katika mazingira magumu na hatarishi.
Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Dodoma Fatma Toffic ameyasema hayo katika halfa ya kukabidhi kadi za bima ya afya kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi waliopo katika kituo cha safina street network zilizotolewa na taasisi ya Miriam supporting society .Aidha amesema jamii inapaswa kujitoa katika kusaidia watoto wanaishi katika mazingira hatarishi huku akiwataka wazazi kuepuka mifarakano ambayo ndio imekuwa chanzo cha kuwa na watoto wengi wa mitaani.
Awali mkurugenzi wa taasisi ya Miriam supporting society Miriam Nteko amesema watoto wanaoishi katika mazingira magumu wamekuwa wakipata changamoto kupata matibabu kutokana na kukosa bima za afya na hivyo kuwaomba wadau wa maendeleo kuunga mkono suala hilo kwa kuendelea kuwakatia bima watoto hao.
Baadhi ya watoto waliopata bima hizo katika kituo cha safina street network akiwemo Amani Abdala ameshukuru kwa kupata bima hiyo na kusema itamsaidia pale atakapo pata matatizo ya kiafya
Jumla ya watoto 142 wamekatika bima za afya za CHF na taasisi ya Miriam supporting society kwa kushirikia na watu waliguswa kuwasaidia watoto hao.
Comments
Post a Comment