Skip to main content

Posts

WANANCHI WASHAURIWA KUFUATA KANUNI ZA UNUNUZI WA ARDHI

        Jamii imetakiwa kufuata taratibu za kisheria katika ununuzi wa ardhi ili kuepuka migogoro ya ardhi inayojitokeza mara nyingi miongoni mwa familia. Rai hiyo imetolewa na Mwanasheria wa Kujitegemea Bwana Goodluck Ludala ambapo amesema migororo mingi ya ardhi inatokana na watu kutokufuata taratibu za kisheria za manunuzi ambapo inaweza kupelekea mtu kupoteza haki yake . Amesema iwapo mtu atapata migogoro ya ardhi anatakiwa kupeleka shauri lake baraza la kata na baada ya uamuzi kutoka mlalamikaji anapaswa kukaza hukumu katika baraza la ardhi la wilaya jambo ambalo watu wengi huwa hawafanyi na kupoteza haki zao. Aidha amesema kumekuwa na baadhi ya watu wanaopuuza hukumu ya mahakama pasipo kukata rufaa ambapo ameeleza kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria na hapo mlalamikaji anapaswa kutoa taarifa katika mahakama iliyotoa hukumu ili hatua zaidi zichukuliwe. Haya Yamejiri ikiwa ni siku chache baada ya Dodoma FM   kupokea kisa cha m...

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WAGANGA WA TIBA ASILI KUBAINI WANAOUA ALBINO

                                           Serikali imeahidi kutoa ushirikiano kwa waganga wa tiba asili katika jitihada za kuwabaini watu wanaojihusisha na mauaji ya vikongwe na watu wenye Ualbino. Hatua hiyo imekuja kufatia hivi karibuni waganga wa tiba asili kuomba kupewa ushirikiano na serikali wakati wa zoezi la kusajili waganga hao ili kubaini waganga wabaya na wazuri jambo ambalo litasaidia kuwabaini waganga matapeli wanaojihusisha na vitendo hivyo. Akiongea na umoja wa waganga wa tiba asili na wakunga ( UWAWATA) pamoja na watu wenye ualbino Mwenyekiti wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania  Mussa Zungu amesema kuwa waganga wabaya wataendelea kuwepo iwapo wateja wabaya watakuwepo hivyo waganga wote watoe ushirikiano kwa vyombo vya dola ili hatua zichukuliwe dhidi ya wale watakaobainika. Naye kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma  G...

SERIKALI :SIYO JUKUMU LETU KUGHARAMIA MAZISHI YA WAZAZI WA WATUMISHI

                                                                          Serikali imesema haina jukumu la kugharamia huduma za mazishi wazazi   wa mtumishi wa umma wanapofariki kutokana na baadhi ya wazazi kuwa na watoto zaidi ya mmoja. Naibu waziri ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEM) Mh. Joseph Kakunda ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri ofisi ya Rais utumishi na utawala bora wakati akijibu swali la Mbunge Kosato Chumi aliehoji ni lini Serikali itawajumuisha wazazi wa mtumishi kama wanufaika wa huduma mbalimbali anazopata mtumishi wa umma. Amesema kwa mujibu wa kanuni za kudumu katika utumishi wa umma inaelekeza huduma za mazishi kutolewa kwa mtumishi mwenyewe pamoja na wategemezi wa nne na uwepo wa kanuni hiyo imesaidia Serikali kue...

SERIKALI YAAHIDI KUPANDISHA MISHAHARA HALI YA UCHUMI ITAKAPOIMARIKA

Waziri wa Nchi ofisi ya Rais utumishi na utawala bora Kapten George Mkuchika amesema Serikali ya awamu ya tano inaendelea kuboresha masilahi ya watumishi wa umma na itapandisha mishahara kwa watumishi hao baada ya hali ya uchumi wa Nchi kuimarika. Waziri Mkuchika ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mh. Catherin Magige aliehoji Serikali ya awamu ya tano ina mikakati gani ya kuwajali watumishi wa umma katika masilahi yao. Kapten Mkuchika amesema Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali katika kuboresha masilahi ya watumishi wa umma kwa kuwapatia mikopo, kuwapeleka mafunzo katika taaluma mbalimbali na zoezi la kupandisha mishahara litafanyika wakati wowote hali ya uchumi wa Nchi utakapo ruhusu. Katika hatua nyingine Kapten Mkuchika amekanusha taarifa za zuio kwa wakurugenzi wa Halimashauri, Manispaa pamoja na Majiji juu ya kuto kuwatangaza wapinzani iwapo wameshinda katika chaguzi mbalimbali kutokana na wak...

WATAMANI KUENDELEZA VITENDO VYA UKEKETAJI WAOGOPA SHERIA

            Pamoja na elimu inayoendelea kutolewa juu ya madhara ya ukeketaji bado kuna baadhi ya maeneo yanaonesha kuendeleza vitendo hivyo vya kikatili kwa wanawake. Dodoma fm imezungumza na baadhi ya wazee wa kimila katika kijiji cha Chikopelo wilayani Bahi ambao wameonesha kutamani kuendeleza vitendo hivyo isipokuwa wanaogopa vyombo vya sheria. Kutokana na imani ya wazee hao kituo hiki kimezungumza na kaimu mganga mkuu mkoa Dodoma Mzee Nasoro ambae amesema mwanamke aliyekeketwa anapata madhara makubwa wakati wa kujifungua ikiwamo kupoteza damu nyingi na hata kupelekea kifo kwa mtoto. Nae mgaguzi msaidizi wa polisi kutoka dawati la jinsia na watoto Lovie Mhena amesema Vitendo vya ukeketaji vimetajwa kuwa ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria ambapo adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 jela. Kutoka mtandao wa wanawake Tanzania bi Sara Mwaga anasema pamoja na tafiti kuonesha dodoma inashika nafasi ya pili katika ukeketaji lakin...

JIJI LA DODOMA LAINGIZWA KATIKA MASHINDANO YA KITAIFA USAFI WA MAZINGIRA

                                                 Uongozi wa jiji la Dodoma umewaomba wananchi  kuendelea kudumisha hali ya usafi ili jiji la Dodoma liweze kuibuka kidedea katika mashindano  ya kitaifa ya usafi wa mazingira. Ushindanishwaji huo utayahusisha majiji yote nchini, jiji la Dodoma likiingia kwa mara ya kwanza katika kinyang’anyiro hicho, na uongozi wa Jiji hilo kuahidi ushindi. Akielezea namna jiji la Dodoma lilivyojipaga   kufanya vizuri katika utunzaji wa mazingra na kupata ushindi, mkuu wa idara ya mazingira na udhibiti wa taka ngumu jiji Dodoma bwna Dickson Kimaro amesema mkoa haupo tayari kumuangusha rais kwa maamuzi yake yenye busara ya kuufanya Mkoa wa Dodoma kuwa jiji, na kuwataka wananchi wote kushiriki kuyatunza mazingira. Aidha bwna Kimaro amewataka watu kuacha kutupa taka kiholela, badala yake watupe katika maeneo y...

KAMANDA MUROTO AWATOA WASI WASI WAKAZI WA DODOMA KUELEKEA SIKUKUU YA IDDI

Katika kuelekea sikukuu ya Eid alfitiri Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limeendelea kuimarisha ulinzi ili kuhakikisha sikukuu inasheherekewa kwa utulivu  pamoja na kuwakamata wahalifu wa makosa mbalimbali. Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake   Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma GILLES MUROTO amesema jeshi la polisi limekuwa likifanya msako wa nyumba kwa nyumba ili kuhakisha wanadhibiti uhalifu na wahalifu na wote watakaokamatwa watafikishwa mahakamani. Kamanda MUROTO amesema jeshi la polisi limekamata zaidi ya watu 25 kwa makosa tofauti tofauti ikiwemo ya uvunjaji, utapeli, bangi na uuzaji wa bidhaa za vipodozi vyenye viambata vya sumu. Sambamba na hayo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu ili jiji la Dodoma liweze kuwa shwari wakati wote. Kwa upande wao wananchi wamesema ni vyema vijana wa kafanya kazi kwa bidii na kuliomba jeshi la Polisi liendelee kuchukua hatua kwa wahalifu wanaowakamata. Na P...