SIMBA WATINGA BUNGENI ,WATAMBULISHWA RASMI MABINGWA WA LIGI KUU
Hii ni kawaida kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano kuikaribisha timu au wana michezo wanaofanya vizuri kwa ajili ya kuwapongeza na kuwapa motisha.
Simba imefanikiwa kutwaa ubingwa huo baada ya kufikisha pointi 68 huku ikisalia na mechi mbili ili kukamilisha ligi.
Naibu Waziri wa TAMISEMI, Joseph Kakunda aliwasifu Wekundu hao kwa uwezo mkubwa walio onyesha huku akisema wataweza kuiwakilisha vizuri nchi katika michuano ya klabu bingwa Afrika mwakani.
Mbali na Kakunda Wabunge Idd Azan wa Ilala, George Lubereje wa Mpwapwa nao hawakusita kuimwagia sifa timu hiyo kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa.
Simba imepitia Dodoma ikitoka Singida iliposhinda bao moja dhidi ya Singida United katika mchezo wa ligi uliofanyika uwanja wa Namfua.
Jana Wekundu hao walicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Dodoma Combine uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 uliopigwa uwanja wa Jamhuri.
Add caption |
Chelsea ambao walikuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo wamemaliza nje ya timu nne bora hivyo msimu ujao watashiriki michuano ya Europa.
Mabingwa watetezi Manchester City wamemaliza ligi hiyo kwa kufikisha pointi 100 kufuatia ushindi wa bao moja dhidi ya Southampton.
Manchester United ilipata ushindi wa bao moja mbele ya Watford huku wakitumia mchezo huo kumuaga nahodha wao Michael Carrick ambaye ametangaza kustaafu soka.
Kwa upande wa Liverpool imeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Brighton wakati Tottenham Hotspur ikipata mabao 5-4 dhidi ya Leicester City.
Matokeo ya mechi zote za EPL
Burnley 1-2 Bournemouth
Crystal Palace 2-0 West Bromwich
Huddersfield 0-1 Arsenal
Liverpool 4-0 Brighton
Man United 1-0 Watford
Newcastle United 3-0 Chelsea
Southampton 0-1 Manchester City
Swansea City 1-2 Stoke City
Tottenham 5-4 Leicester City
West Ham United 3-1 Everton
Huddersfield wabaki ligi kuu huku Gurdiola akiivunja rekodi ya Mourinho
Alama moja katika uwanja wa Stamford Bridge umeihakikishia klabu ya Huddersfield kuwepo katika ligi kuu nchini Uingereza katika msimu ujao, matokeo ya leo yanawafanya kufikisha alama 37 katika msimamo wa ligi alama ambazo zinawahakikishia uwepo katika ligi kuu.
Habari nyingine kubwa katika mchezo wa leo ni namna ambavyo kocha wa Chelsea Antonio Conte alikipanga kikosi chake akimuacha Eden Hazard nje pamoja na Olivier Giroud na alama moja waliyoipata hii leo inawaweka katika hatihati kushiriki Champions League msimu ujao.
Suluhu ya leo ya Huddersfield inamaanisha kwamba timu zote zilizopanda daraja msimu huu zinabaki ligi kuu na hii ikiwa ni mara ya tatu katika historia ya Epl kwa jambo kama hili kutokea ambapo ilishatokea msimu wa 2001/2002(Blackburn, Fulham na Bolton) na ikatokea pia
2011/2012(Swansea, Norwich na Qpr)
.
Kwingineko mabao mawili ya Riyad Mahrez na moja la Jamie Vardy yalitosha kuiua Arsenal bao 3 kwa 1, ambapo matokeo haya yanawafanya Arsenal kuwa timu ambayo inaongoza kwa matokeo mabovu ugenini kuliko timu yeyote katika ligi kuu 5 kubwa barani Ulaya kwa mwaka 2018.
Manchester City waliipiga Brighton & Hove Albion mabao 3 na hii kuwafanya City kushinda michezo 31 katika msimu huu wakiifikia rekodi ya Tottenham waliyoiweka 1960/1961 ya kushinda idadi ya michezo kama hiyo katika ligi, lakini pia Gurdiola anakuwa ameivunja rekodi ya Jose Mourinho ya kumaliza ligi akiwa na alama nyingi ambapo Pep amefikisha 97, huku Mou alifikisha 95 msimu wa 2004/2005.
SIMBA WAANZA SAFARI KUELEKEA SINGIDA, KIKOSI KITAPITA BUNGENI KUPOKEA BARAKA ZA MCHEZO
Kikosi cha Simba kimeanza safari ya kuelekea Singida kwa ajili ya mtanange wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Singida United.
Simba itapitia katika Makao Makuu ya nchi, Dodoma, kuweka kambi fupi kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea mjini Singida.
Taarifa kwa mujibu wa Meneja wa kikosi hicho cha wekundu wa Msimbazi, Richard Robert, amesema kuwa kikosi kitapita jijini hapo ili kuweka kambi fupi kabla ya kuendelea na safari.
Inaelezwa kuwa Simba wamepanga kupitia Bungeni kwa ajili ya kupata baraka za kuelekea mechi yao na Singida itakayopigwa Mei 12 kwenye Uwanja wa Namfua.
Tayari kikosi hicho kipo njiani hivi sasa kuelekea jijini humo na kesho kitaanza tena safari ya Singida.
Kocha wa Prisons aivua ubingwa Yanga
Kuelekea mchezo wa VPL kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Yanga, Kocha mkuu wa Prisons Abdallah Mohamed ‘Bares’ ameivua ubingwa Yanga na kuipa Simba nafasi ya kushinda taji la ligi kuu msimu huu.
Bares amesema Simba inahitaji pointi moja kuwa bingwa wa ligi huku ikiwa na mechi tatu jambo ambalo linaiondoa Yanga katika mbio za ubingwa wa VPL 2017/18.
“Tunaona tayari Yanga ameshaondoka kwenye mbio za ubingwa kwa sababu Simba anahitaji pointi moja kuwa mabingwa, mchezo dhidi ya Yanga ni muhimu sana kwetu kupata pointi tatu.”
“Nadhani Yanga wanakuja wakiwa wanajiandaa zaidi kwa mechi yao ya kimataifa, huu utakuwa mchezo wa kuandaa mazoezi ambayo yatawasaidia na mapungufu ambayo wameona kwenye mchezo waliofungwa 4-0 USM Alger. Nadhani kikubwa mwalimu atatazama hicho zaidi.”
“Kikosi changu kipo vizuri isipokuwa tutamkosa mchezaji mmoja Salum Kimenya ambaye anakabiliwa na kadi tatu za njano kwa hiyo hatutaweza kumtumia lakini tuna vijana wengi ambao wako vizuri na tunaamini watafanya vizuri.”
“Kila timu imejipanga kwa namna yake, sisi tumejipanga kukamata nafasi za juu nadhani Yanga kama kawaida yake haitaki kushuka chini zaidi inataka kubaki palepale nadhani mchezo utakuwa ni mkubwa lakini tuangalie dakika 90 zitaamua nini.”
“Tunacheza na Yanga ambayo jina lake ni kubwa lakini timu ya kawaida kabisa, sisi kama unavyoona mwenendo wetu sio mbaya kwa hiyo tunataka kuendeleza hiyo rekodi yetu.”
MWENYEKITI ABAJALO AFUNGULIWA KUJIHUSISHA NA SOKA, MMOJA RUFAA YAKE YATUPILIWA MBALI
Kamati ya Rufaa ya Maadili imeitupilia mbali rufaa ya Dustan Mkundi Ditopile na kuiagiza Sekretariati kulipeleka suala kake katia vyombo vya ulinzi kwa uchunguzi zaidi.
Dustan alifungiwa kutokana na kuwasilisha fomu ya mapato tofauti na fomu halisi ya Bodi ya Ligi.
Wakati huohuo Mwenyekiti wa Abajalo FC na mjumbe wa Bodi ya Ligi alikiri kutoa maneno makali mbele ya vyombo vya habari akiwa kama kiongozi.
Kutokana na kukiri kwake, Kamati imemfungulia kifungo cha kutojihusisha na soka Edgar Chibula na kumpa onyo kali.
NIYONZIMA AMWAHIDI AHADI HII KOCHA WAKE
Baada ya kurejea uwanjani, kiungo wa Simba, Haruna Niyonzima raia wa Rwanda amemuahidi makubwa kocha wake Pierre Lechantre kwa kusema kuwa ni nafasi nzuri kwake kuonyesha kiwango baada ya kupata nafasi ya kucheza.
Niyonzima alikaa nje ya uwanja tangu na kukosa baadhi ya mechi baada ya kuumia enka kulikomsababishia kupelekwa nchini India kwa matibabu kabla ya kurejea kikosini.
Kiungo huyo machachari alipewa nafasi ya kucheza kwa mara ya kwanza tangu arudi majeruhi katika mchezo dhidi ya Njombe Mji, Jumatatu wiki hii kwenye Uwanja wa Sabasaba, akichukua nafasi ya Shiza Kichuya dakika ya 81, ambapo Simba ilishinda mabao 2-0 yaliyofungwa na John Bocco.
Niyonzima alisema, amefurahi kuona amerejea uwanjani kwa mara nyingine baada ya kukaa nje kwa muda mrefu.
YANGA YATUA MOROGORO KWA AJILI YA DICHA
Mabingwa
watetezi wa Ligi Kuu Bara, Young Africans, wameweka tena kambi nyingine
maalum mjini Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la
Shirikisho Afrika dhidi ya Welayta Dicha FC.
Yanga
ilitua Morogoro jana ikitokea mkoani Singida kucheza mchezo wa Kombe la
FA dhidi ya Singida United kwenye hatua ya robo fainali ambapo
iliondolewa kwa changamoto ya mikwaju ya penati (4-2).
Kikosi
hicho kimeshindwa kufika Dar es Salaam na kuamua kuishia Morogoro kwa
ajili ya mawindo dhidi ya Welayta Dicha FC kutoka Ehtiopia inayotaraji
kuwasili nchini wiki hii.
Yanga
itacheza na Waethiopia hao Jumamosi ya Aprili 7 2018 katika Uwanja wa
Taifa Dar es Salaam, kabla ya kurudiana nao huko Ethiopia baada ya wiki
moja mbele.
KUMBE KOCHA NJOMBE NI MJANJA, AMETUMIA MBINU HII KUIMALIZA SIMBA LEO
Wakati pambano la Ligi Kuu Bara likisubiriwa jioni ya leo kati ya Njombe Mji FC dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe, Kocha Msaidizi wa timu ya Njombe, Mrage Kabange, ameeleza mbinu alizoziandaa kupata matokeo.
Mrage
ameeleza kuwa walilazimu kupeleka nusu kikosi mjini Shinyanga kwa ajili
ya mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Stand United na kubakisha
kingine mjini Njombe.
Kocha
huyo amesema iliwabidi wafanye hivyo ili wapate nguvu ya kupambana na
Simba kwenye ligi kutokana na hali ya kikosi chao kuwa mbaya kwasababu
wako kwenye mazingira ya kushuka daraja.
Taarifa
zinaeleza kuwa kikosi cha Njombe kilichopelekwa Shinyanga kilikuwa na
wachezaji wengi wa akiba na waliosalia Njombe walikuwa ni wale wa kikosi
cha kwanza.
Uamuzi
huo ulifanywa ili kuipa timu nguvu ya kupigania alama tatu muhimu dhidi
ya Simba ambayo imekosa ubingwa wa ligi kwa miaka mitano sasa.
Mechi hiyo inachezwa leo Uwanja wa Sabasaba kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni.
ZLATAN AWASILI MAREKANI NA KUPOKELEWA KWA SHANGWE NA MASHABIKI WA LA GALAXY
Aliyekuwa Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, amewasilini jijini California, Marekani, na kupokelewa na mashabiki wa LA Galaxy.
Zlatan alitangaza kuhamia Marekani baada ya kukubaliana na klabu yake ya zamani kuvunja mkataba kufuatia kuwa nje ya dimba kwa muda mrefu sababu ya majeraha.
Mshambuliaji huyo atasaini mkataba wa kuicheza LA Galaxy iayoshiriki ligi kuu nchini humo na inaelezwa anaweza kumaliza maisha yake ya soka akiwa na klabu hiyo.
UCHUNGUZI WA URAI WA KIDAO BADO UNAENDELEA
Idara ya uhamiaji nchini bado inaendelea kuchunguza uraia wa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF Wilfred Kidao, afisa habari wa uhamiaji Ally Mtanda amesema uchunguzi bado unaendelea na utakapo kamilika watatoa taarifa rasmi.
“Bado tunaendelea na suala lake la uchunguzi na litakapokuwa tayari tutawaarifu, masuala ya uchunguzi hatuwezi kuyaweka wazi hadi pale tutakapokuwa tumekamilisha ndipo mambo yote yatakuwa hadharani.”
“Wanamicheo wawe na uvumilivu muda sio mrefu mambo yote tutayaweka wazi.”
Mara kadhaa Kidao amekuwa akihojiwa na idara hiyo kutokana na kinachoelezwa kuwa ni kuchunguzwa uraia wake.
YANGA YAMKANA MUDATHIR
Mudathir Yahya anazidi kutawala kwenye vichwa vya habari za michezo akihusishwa kujiunga na Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa taji la VPL.
Kiungo huyo anaecheza kwa mkopo Singida United amemaliza mkataba wake na klabu ya Azam hivyo kwa sasa ni mchezaji huru na anaweza kujiunga na timu yoyote atakayoamua mwenyewe.
Mara baada ya uongozi wa Azam kupitia msemaji wake Jafar Idd kutangaza kumruhusu mudathir kuendelea na maisha yake ya soke sehemu nyingine, Yanga inatajwa kuanza kuiwinda saini ya mchezaji huyo wa Zanzibar Heroes na Taifa Stars.
Mwenyekiti wa kamati ya mashindano Yanga Hussein Nyika amesema hadi sasa klabu yao haijaongea na mchezaji yeyote wala hawajafanya usaji wa aina yoyote.
“Hakuna kitu kama hicho sisi (Yanga) tunaelekeza nguvu zetu kwenye mashindano, hatujafika kipindi cha usajili. Yanga inafanya usajili kwa taratibu zake, baada ya mashindano kumalizika lazima mwalimu atuletee ripoti yake anahitaji maeneo gani yajazilizwe hapo ndipo tutaingia msituni kwa ajili ya usajili.”
“Hadi sasa hivi hatujaongea na mchezaji wa aina yoyote na hatujafanya usajili wa aina yoyote. Hatuwezi kufanya usajili kwa sababu mchezaji yupo huru, usajili wetu huwa tunafanya baada ya kupokea ripoti ya mwalimu na mapendekezo yake. Mwalimu ndio anafanya usajili sisi tunatekeleza ambayo mwalimu anaagiza.”
Uongozi wa Singida United umesema, pamoja na Mudathir Yahya kumaliza mkataba na Azam wao wana mipango nae na huenda wakaingia mkataba wa muda mrefu na mchezaji huyo
WAMBURA :KESHO KUJUA MBIVU NA MBICHI
Kamati ya rufaa ya maadili ya shirikiso la soka Tanzania TFF imetangaza kukutana Jumamosi kwa ajili ya kusikiliza rufaa ya aliyekuwa makamu wa Rais wa shirikisho hilo Michael Wambura aliyefungiwa maisha kujishughulisha na masuala ya soka.
Kaimu afisa habari wa TFF Clifford ndimbo amethibitisha kuhusiana na taarifa hiyo.
“Kamati ya rufdaa ya maadili inataraji kukaa Jumamosi ya Machi 31 ambapo itakuwa saa 5 asubuhi, pamoja na mambo mengine pia itasikiliza rufaa ya Michael Wambura ambaye alikata rufaa.”
“Anaruhusiwa kuja kutoa utetezi wake kwa njia ya mdomo, maandishi au kuleta vielelezo vyote vya utetezi wake pia anaweza kuleta mwakilishi akiwa na barua ya uwakilishi au anaweza kuamua kutokuja kabisa.”
“Tayari wito wake ameshapelekewa na bila shaka atakuwa amesha upokea, kuelekea katika shauri hilo siku ya Jumamosi gharama zitakuwa juu yake mwenyewe.”
Wakili wa Wambura Emanuel Muga amesema mteja wake amepokea wito kutoka kamati ya rufaa ya maadili na atakwenda kutetea haki yake mbele ya kamati hiyo.
“Ni kweli Michael Wambura amenieleza kwamba amepata wito na wito huo ni kwa ajili ya kikao cha Machi 31 saa 5 asubuhi pale TFF atakapoenda kusikilizwa.”
“Wambura amesema yupo tayari kwenda kutetea haki yake mbele ya kamati na ana hoja zake na amethibitisha kwamba atakwenda.”
MKUTANO MKUU YANGA KUFANYIKA MEI 5 DAR ES SALAAM KUJADILI MUSTAKABALI MPYA WA KLABU
KLABU ya Yanga inatarajiwa kufanya Mkutano wake Mkuu wa mwaka Mei 5 mwaka huu katika ukumbi utakaotajwa baadaye mjini Dar es Salaam.
Mkutano huo ni matokeo ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya Yanga kilichofanyika Jumapili iliyopita mjini Dar es Salaam chini ya Kaimu Mwenyekiti, Clement Sanga ambacho kimewataka wanachama kujindaa kwa ajenda zitakazotangazwa baadaye.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Yanga SC, Charles Boniface Mkwasa alipozungumza na Waandishi wa Habari makao makuu ya klabu, Jangwani mjini Dar es Salaam.
Mkwasa, mchezaji na kocha wa zamani wa Yanga pamoja na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars amesema kwamba mkutano huo utakuwa maalum kwa wanachama kujadili masuala mbalimbali na kwa ujumla mustakabali wa klabu.
AZAM YATANGAZA KUACHANA NA MUDATHIR YAHAYA
Uongozi wa klabu ya Azam FC umetangaza kuwa mchezaji wake, Mudathir Yahaya, yupo huru kuelekea sehemu nyingine baada ya kumaliza mkataba wake.
Kupitia Afisa Habari wa Azam FC, Jaffer Idd, amesema mchezaji huyo yupo huru hivi sasa na kama timu nyingine ikimuhitaji, ruksa kumsajili.
Yahaya aliondoka Azam FC na kutimkia Singida United kwa mkopo Julai 17 2017 baada ya mkataba wake wa miezi mitatu uliokuwa umesalia ndani ya Azam kumalizika.
Mpaka sasa Yahaya yuko Singida United akijiandaa na wenzake kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho utakaopigwa Aprili Mosi 2018 dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Namfua.
Wachezaji wa Simba waliokuwa wanaitumikia Taifa Stars wanatarajiwa kujiunga na kikosi cha Simba kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Njombe Mji.
Simba inajiandaa kucheza na Njombe Aprili 3 2018 katika Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe, mchezo ambao ulikuwa ni wa kiporo.
Wachezaji hao waliokuwa Stars ni Erasto Nyoni, Aishi Manula, Shiza Kichuya, Shomari Kapombe pamoja na Said Ndemla.
Simba inaendelea na mazoezi jioni ya leo kwenye Uwanja wa Boko Veterani kabla haijakabiliana na Njombe Mji FC Aprili 3 2018.
LIGI YA WILAYA YA DODOMA MJINI MAMBO NI MOTO SASA
baada ya semini ya hapo jana ya viongozi wa vilabu shiriki wa ligi ya wilaya ya Dodoma chama cha soka wilaya ya Dodoma mjini Dufa kimetoa ratiba rasmi pamoja na makundi ya ligi hiyo ambayo inashirikisha vilabu 20
omaroo Omary materazi ni katibu msaidizi wa dufa anabainisha juu ya malengo ya semina ya jana pamoja na ratiba nzima ya ligi ya wilaya ya dodoama mjni ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi aprili 4 2018
Na Selemani Juma
BINGWA WA MKOA WA DODOMA NI GWASSA NATO
Baada ya kutangaza bingwa hapo jana wa ligi ya mkoa wa Dodoma Chama cha soka mkoani Dodoma dorefa kimeshukuru wadau pamoja na wanamichezo wote ambao walijitokeza tangu lingi hiyo ianze mpaka kufiko ukomo hivi karibuni
Akizungumza na sport bomba Katibu wa chama cha soka mkoani Dodoma dorefa ham isi kisoi amesema kuwa bingwa wa mkoa wa Dodoma ni Gwassa nato lakini tangu kwa kuanza kwa ligi hiyo kumekuwa na mwitikio wa wadau kuunga mkono licha ya changamoto zilizojitokeza katikati mwa ligi hiyo
Hamisi kisoi huyu hapa akibainisha namna walivyojipanga kuhakikisha ligi ijayo inakuwa na maandalizi ya kutosha tofauti na msimu huu
Na Selemani Juma
KOCHA MTIBWA SUGAR :DFC WANAWEZA KUPANDA LIGI KUU
Na leo katika uwanja wa ccm jamhuri kulikuwa na mchezo wa kirafiki baina ya klabu ya Dfc dhidi ya mtibwa sugar kutoka mkoani morogoro.
Mchezo huo umekamilika jioni ya leo kwa kushuhudia Mtibwa sugar wakiibuka na ushindi wa goli 2 dhidi ya sifuri kwa wenyeji wao Dfc
Baada ya mchezo huo kocha wa mtibwa sugar zubery katwilla amesema kuwa mchezo wao huo ni miongoni mwa maandalzi ya mchezo wao wa kombe la shirikisho dhidi ya azam huku pia akitoa somo kwa klabu ya dfc namna gani wafanye ili waweze kufanikiwa katika harakati za kupanda ligi kuu
Pia tuliweza kumtafuta katibu wa klabu ya dfc Super Fortu kujua baada ya mchezo huo wa leo klabu wanamipango gani katika kuhakikisha wanacheza michezo mingine kama ilivyokuwa ahadi yao kwa wadau wa soka na mashabiki wa dfc .
Clip super fortu
MKUDE :NJE WIKI MOJA
Kiungo
wa klabu ya Simba, Jonas Mkude, imearifiwa anaweza akakosekana dimbani
kwa takribani wiiki moja kufuatia kuumia juzi mazoezini.
Simba
imekuwa ikifanya mazoezi katika Uwanja wa Boko Veterani jijini Dar es
Salaam ambapo hivi sasa inajiandaa na mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Njombe
Mji FC utakaopigwa Aprili 3 2018.
Kwa
mujibu wa Daktari wa timu, Yassin Gembe, amesema Mkude anaweza
akachukua wiki moja badala ya siku mbili au tatu zilizotajwa awali.
Mkude aliumia mguu wakati wa mwazoezi baada ya kukutana na Mzamiru Yassin wakati wakiwania mpira.
TFF YATUMA MAOMBI TLS IKIOMBA WAKILI WA WAMBURA APIGWE 'STOP' MARA MOJA
Shirikisho
la Soka nchini (TFF), limekiomba Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS),
kumzuia Wakili Emmanuel Muga, kumuwakilisha aliyekuwa Makamu wa Rais wa
TFF, Michael Richard Wambura, katika rufaa yake inayotegemewa
kusikilizwa muda wowote kuanzia wiki hii.
Taarifa
hiyo iliyosambaa inaeleza kuwa Wakili Emmanuel Muga alikuwa ana mkataba
na TFF, na suala la Ndug. Wambura lilitendeka enzi za uhai wa mkataba
wake.
TFF
inaiomba TLS imuagize Muga asitishe mara moja uwakilishi wake katika
mashauri mengine yanayoihusisha TFF na viongozi wake, wanachama au
walalamikaji wengine ili kuondoa mgonagano huu wa kimaslahi.
Wakili
Muga anamuwakilisha Wambura aliyefungiwa kujihusisha na masuala ya soka
baada ya TFF kugundua kuwa aliutumia kinyume na matwaka fedha za
shirikisho hilo, pamoja na makosa mengine mbalimbali.
=======================================================
Kikosi cha Taifa Stars kinashuka Uwanjani 'Mustapha
Tchaker Stadium' kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Algeria jioni
ya leo huko Blida, nchini humo.
Mchezo huo ambao ni wa kalenda ya FIFA, utakuwa unaipa nafasi Tanzania ya
kulipiza kisasi baada ya kupoteza kwa mabao 7-0 wakati timu hizo zilipokutana
mara ya mwisho 2015.
Tanzania ilifungwa idadi hiyo ya mabao wakati wa kuwania kufuzu kuelekea
michuano ya Kombe la Dunia kuelekea Urusi mwaka huu.
Licha ya kufungwa, timu zote hazijafanikiwa kufuzu kushiriki michuano hiyo
inayotarajia kuanza miezi kadhaa ijayo.
Lakini wakati hayo yakijiri ni kwamba shirikisho la soka
tz limeanza mchakato wa kutafuta kocha mpya wa kukinoa kikosi cha starz
kutokana mkataba wa salum mayanga kufika ukingoni
====================================================
Mchezo huo ambao ni wa kalenda ya FIFA, utakuwa unaipa nafasi Tanzania ya kulipiza kisasi baada ya kupoteza kwa mabao 7-0 wakati timu hizo zilipokutana mara ya mwisho 2015.
Tanzania ilifungwa idadi hiyo ya mabao wakati wa kuwania kufuzu kuelekea michuano ya Kombe la Dunia kuelekea Urusi mwaka huu.
Licha ya kufungwa, timu zote hazijafanikiwa kufuzu kushiriki michuano hiyo inayotarajia kuanza miezi kadhaa ijayo.
Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa Tanzania
(Takukuru), imeieleza mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu kuwa imeshakamilisha upelezi wa kesi ya Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey
Nyange 'Kaburu' na wapo tayari kuanza
kusikilizwa.
Aveva leo ameshindwa kuhudhuria tena mahakamani katika
kesi yake utakatishaji fedha
inayomkabili ikiwa ni mara ya saba mfululizo kutokana kutokana na kulazwa
katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
kufuatia hali yake ya kiafya kutokuwa nzuri.
Aveva anakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi,
kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha kiasi cha dola 300,000 za Kimarekani akiwa
na makamu wake wa rais Geofrey Nyange
'Kaburu'.
Katika kesi hiyo ambayo itakuwa ikisikilizwa mbele
ya Hakimu Mkazi wa Makahama ya Kisutu, Thomas Simba badala ya Victoria Nongwa ambapo wakili wa Takukuru,
Nassor Katuga ameiambia mahakama hiyo kwamba kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya
kutajwa lakini wameshakamilisha upepelezi hivyo wapotayari kuendelea kwa hatua
ya kuanza kusikilizwa.
Katuga alisema
kuwa kusema kuwa lakini wapokea taarifa kuwa mshitakiwa namba moja (Aveva)
ameshindwa kufika mahakamani kwa kuwa anaumwa na melazwa Muhimbili nabadala
yake yupo Kaburu peke yake ambaye ni mshitakiwa namba mbili.
Kwa upande wa
hakimu Simba alisema kuwa ni vyema kufuatilia hali yake kwa kuwa kesi
ipo tayari kusilizwa ili iweze kuendana na muda kutona na kuwa ni ya muda mrefu
ambapo amepanga kuanza kusilizwa Aprili
5, mwaka huu.
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@
Baada ya Yanga kupangwa na Welayta Dicha ya Ethiopia
kwenye Kombe la Shirikisho Afrika na CAF jana Machi 21 2018, timu hiyo imeguwa
gumzo kwa watu.
Welayta Dicha ni timu inayoshiriki Ligi Kuu Ethiopia na
msimu huu ipo nafasi ya nane kwenye Msimamo wa Ligi Kuu nchini humo ikiwa
imecheza jumla ya michezo 15 na kujikusanyia alama 19.
Kupitia mitandao mbalimbali na hata vijiweni baadhi ya
watu wamekuwa wakihoji kuhusiana na timu hii kama itaweza kusonga mbele
kutokana na kutokujulikana kwake zaidi.
Kuna baadhi pia wapo wanaoona kama Yanga imepata mteremko
wa kupita kirahisi kwa nafasi iliyopo kwenye Msimamo wa Ligi.
Yanga imepangwa kucheza na klabu hiyo baada ya kuondoshwa
kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, kufuatia kichapo cha mabao 2-1.
====================================================
Gor Mahia (Kenya), Young Africans (Tanzania) na Rayon Sport
(Rwanda) zimefahamu wapinzani wake katika mechi za mtoano zitakazoamua timu za
kushiriki hatua ya makundi ya kombe kwa shirikisho la vilabu barani Afrika.
Katika droo iliyochezeshwa jana mjini Cairo, Young
Africans imepangwa kucheza na Wolaita Dicha ya Ethiopia, Rayon Sport itacheza
dhidi ya Costa do Sol ya Msumbiji na Gor Mahia dhidi ya Supersport United ya
Afrika Kusini.
Kwenye mechi za kwanza za hatua hiyo, timu zote tatu
zitakuwa nyumbani kati ya Aprili 6-8 na kwenda ugenini Aprili 17-18 na endapo zitafuzu
basi moja kwa moja zitaingia kwenye droo ya hatua ya makundi.
===================================================
Bingwa wa uzito wa juu katika mchezo wa Ngumi Anthony
Joshua AJ wa Uingereza amemuonya Joseph Parker wa New Zealanand ambaye ni
mpinzani wake katika pambano litakalofanyika machi 31 mjini Cardiff.
Katika maneno yake, AJ amemwambia Joseph ajiandae na
pambano gumu ambalo litaamua bingwa wa mkanda wa WBO.
Katika hatua nyingine AJ amekubali uwezo mkubwa wa
kupigana alionao Joseph.
===============================================
Mshambuliaji wa Manchester United, Alexis Sanchez,
amesema alitarajia mambo kwenda sawa baada ya kujiunga na Manchester United
January 2018.
Mchezaji huyo ameeleza hayo baada ya kuona mambo yanaenda
tofauti na alivyotarajia mpaka sasa tangu aondoke Arsenal na kutua Old
Trafford.
Sanchez mpaka sasa amepata nafasi moja tu ya kucheka na
nyavu katika michezo 10 aliyoichezea Manchester United tangu ajiunge.
Aidha, Mshambuliaji huyu amekiri kuwa anahitaji kupambana
zaidi ili kuweza kuzoea maisha mapya ndani ya United ambayo bado ni klabu ngeni
kwake hivi sasa.
BAADA YA KUBEBA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA URENO, RONALDO ASEMA YEYE NI BORA SIKU ZOTE
Kwa mara ya pili mfululizo, Mshambuliaji wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo, ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2017 katika taifa lake maarufu kama Quinas de Ouro.
Tuzo hiyo ambayo alikabidhiwa jana Jumatatu, Ronaldo alikuwa akiiwania na wachezaji Bernardo Silva wa Manchester City pamoja na Golikipa wa Sporting CP ya Ureno, Rui Patricio.
Baada
ya kuzawadiwa, Ronaldo alisema yeye anaamini bado ni bora na ataendelea
kuwa hivyo, hata kama atasemwa kwa namna gani, na hilo atazidi
kuwaonesha Uwanjani.
"Naamini kuwa mimi ni bora, vyovyote watakavyosema mimi nitawaonesha ubora wangu Uwanjani" alisema.
Ronaldo
ametwaa tuzo hiyo kutokana na mafanikio makubwa ya soka mwaka 2017 kwa
kuweza kuisaidia Real Madrid kubeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na
kuchukua ubingwa wa La Liga.
Mbali
na mataji hayo, Ronaldo pia alifanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa
dunia 'Ballon d'Or kwa mara ya pili mfululizo na kufanya awe na jumla
ya tuzo 5 sawa na Lionel Messi.
MAKOCHA WAFUNGIWA BAAADA YA VURUGU
Kamati tendaji ya chama cha soka mkoani dodoma imewafungiwa miezi sita na kuwatoza faini makocha wa vilabu vya gwassa nato ya chang’ombe na Watumishi ya mpwapwa kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo tukio la vurugu katika mchezo wa Gwassa dhidi ya watumishi
Kupitia
taarifa ya DOREFA kwa vyombo vya habari imesema kuwa katika mchezo wa
gwassa dhidi ya watumishi uliofanyika tarehe 18 mwezi wa 3 mwaka 2018
wameabaini matukio mbalimbali,1mashabiki kufanya vurugu,walimu wa timu
mbili hizo kugombana,kumtukana msimamizi wa kituo,kocha msaidizi wa timu
ya watumishi kuzuia wachezaji kutoendelea na mchezo,timu ya watumishi
kugoma kuendelea na mchezo na baadhi ya wachezaji kujihusisha na
vurugu.
Kupitia kamati tendaji ambayo imekata hapo juzi
wamatoka na maamuzi ya timu ya gwassa pamoja na timu wa watumishi
vimetozwa faini ya shilingi laki moja kila mmoja kutoka na msahbiki wake
kuhusika na vurugu na fedha hizo zinatakiwa kulipwa kabla ya michezo
inayofutia.
Baada ya taarifa hiyo nilimtafuta mtendaji mkuu wa
chama cha soka mkoani dodoma Hamisi kisoi Amesema kuwa kutoka na maamuzi
hayo ,wataendelea kuhakikisha wanasimamia ligi hiyo kwa misingi ya
usawa na uwazi na haki mpaka bingwa hapatikane
Pia tumezungumza
na kocha wa Gwsaa nato Juma ikaba ambaye amefungiwa miezi Sita na
kutozwa faini ya shilling laki moja amesema kuwa kutoka na maamuzi hayo
ameyapokea hana budi kukubali juu ya hilo
Wadau wa soka
wanasemaje juu ya maamuzi haya,super fortu ambaye pia ni katibu wa timu
ya DFC yeye ni mdau wa soka ametoa pongezi kwa chama cha soka mkoani
dodoma juu ya maamuzi hayo
NA SELEMANI JUMA
LIGI YA DUFA KUANZA APRIL 4
Ligi ya wilaya ya dodoma mjini maarufa kama ligi ya DUFA inatarajia kuanza kutimua vumbi kuanzia april 4 kwa kushirikisha vilabu 20 vya wilaya ya dodoma mjini
Kupitia
taarifa kutoka kwa katibu wa Msaidizi wa DUFA Omaroo amesema kuwa kwa
sasa DUFA wapo kwenye mipango ya mwisho ya kuhakikisha vilabu
vinakamilisha ada ya ushiriki kabla ya kuanza kutoa semina kwa vilabu
,viongozi na waamuzi ambao watacheza ligi hiyo.
Amesema kuwa tayari wameshafanya vikao vitatu ambavyo vimelenga kumaliza mchakato wakuanza ligi ya wilaya ya dodoma mjini
Omaroo
amesema ligi ya msimu hii itafanyika kwa mtindo wa siku tatu toafuti na
msimu uliopita ambapo utachezwa kwa siku jumamosi,jumapili pamoja na
jumatano hiyo ni kutokana na vilabu kukosa fedha za kumuda kila siku
kushiriki ligi.
Aidha
amesema kiwanja ambacho kitatumika katika ligi hiyo ni uwanja wa Ccm
Jamhuri ambao utatumika kwa siku zote tofauti na wiki ya maandalizi ya
siku ya muungano ambapo watawajulisha vilabu kuhusu uwanja utakaotumika
kuchezwa kwa wiki ya muungano.
NA SELEMANI JUMA KODIMA
KILA LA HERI SIMBA NA YANGA MISRI NA BOTSWANA LEO…TUNAWATAKIA USHINDI NA KUSONGA MBELE
WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye michuano ya Afrika, Simba na Yanga leo wapo ugenini kwa michezo ya marudiano ya hatua ya 32 Bora.
Yanga
watakuwa wageni wa Township Rollers Uwanja wa Taifa mjini Gaborone,
Botswana kuanzia Saa 10:45 jioni katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa na
Simba watakuwa wageni wa Al Masry Uwanja wa Port Said nchini Misri
kuanzia Saa 2:30 usiku.
Yanga
wanahitaji lazima ushindi wa mabao 2-0 ili kwenda hatua ya makundi,
baada ya kufungwa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza Jumanne ya wiki iliyopita
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba SC wanataka ushindi wowote, hata wa 1-0 ili kusonga mbele katika hatua ya mwisho ya mchujo baada ya sare ya kufungana mabao 2-2 kwenye mchezo wa kwanza Dar es Salaam.
Yanga
ikiitoa Rollers itakwenda hatua ta makundi ya Ligi ya Mabingwa, ambayo
kihistoria itakuwa mara yake ya pili baada ya mwaka 1998, lakini tolewa
itaingia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la
Shirikisho.
Simba
SC ikishinda leo itacheza na moja ya timu zilizotolewa kwenye Ligi ya
Mabingwa Afrika kuwania nafasi ya kucheza Kombe la Shirikisho, lakini
ikitolewa itarejea nyumbani moja kwa moja.
Kila la heri wawakilishi wetu. Mungu zibariki Simba na Yanga. Mungu ibariki Tanzania. Amin.
BREAKING: RAIS WA FIFA ATHIBISHA RASMI KUTUMIKA KWA VAR KOMBE LA DUNIA 2018 RUSSIA
Teknolojia
ya Video Assistant Referees (VAR), imethibitishwa rasmi kutumika kwenye
michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu nchini Russia.
Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino amethibisha hilo leo.
Majaribio ya teknolojia hiyo ya VAR yalifanyika katika nchi za Germany na Italy katika msimu huu.
Infantino
amesema inabidi mpira wa soka uishi kuendana na wakati hivyo amefikia
hatua hiyo ili kuwasaidia Waamuzi kutoka maamuzi sahihi Uwanjani.
"Tunahitaji
kuishi kuendana na wakati, tulihitaji kuwapa Waamuzi vifaa ambavyo
vitawasaidia kutoa maamuzi sahihi Uwanjani" alisema.
KISA MESSI, LAWAMA ZOTE ATUPIWA MLINDA MLANGO THIBAUT COURTOIS
Baada
ya Chelsea kuondoshwa kwenye Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya FC,
Barcelona kwa jumla ya mabao 3-0, lawama zote zinatupiwa kwa mlinda
mlango, Thibaut Courtois.
Kupitia
mitandao mbalimbali mashabiki wengi wa Chelsea wamemuandama Golikipa
huyo, wapo wengine wanasema amechoka na pengine aondoke klabuni hapo na
akatafute maisha mahala pengine.
Courtois aliruhusu mabao matatu ya Lionel Messi aliyefunga mawili, pamoja na Oeusman Dembele aliyefunga moja na jumla kuwa 3-0.
Mabao
aliyofungwa na Messi yamekuwa gumzo zaidi, kutokana na baadhi kudai
Courtois angeweza kuokoa mipira hiyo iliyopita katikati ya miguu yake.
Kitendo cha kuruhusu mabao hayo kimekuwa kero kubwa kwa mashabiki wa Chelsea ambao timu yao ishatolewa rasmi kwenye mashindano.
Baada ya Barcelona kufuzu kuingia robo fainali, droo ya timu zitakazokutana kwenye hatua hiyo inataraji kupangwa kesho.
Timu zilizofuzu ni Liverpool, Real Madrid, Manchester City, Bayern Munich, AS Roma, Sevilla, Juventus na FC. Barcelona.
RASMI WAMBURA AFUNGIWA MAISHA KUTOJIHUSISHA NA SHUGHULI ZA SOKA
Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemfungia maisha kutojihusisha na shughuli za Soka Makamu wa Rais wa TFF, Michael Wambura.
Wambuwa amefungiwa kutokana na kupokea fedha zisizo halali kiasi cha Shilingi milioni 84, kugushi nyaraka za malipo, na kula njama kulipwa fedha na waliokua viongozi wa TFF Jamal Malinzi na Selestin Mwesigwa.
KOCHA MRUNDI WA SIMBA ANAAMINI WATAFANYA HIVI MAAJABU MISRI KWA AL MASRY
Kocha Msaidizi wa Simba Mrundi, Masoud Djuma amesema nguvu zao wamezielekeza kwenye mchezo wao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Al Masry ya Misri na baada ya hapo wanarejea kwenye Ligi Kuu Bara kupambana na Yanga.
Kauli hiyo ameitoa kocha huyo baada ya Yanga kuwafikia kwa pointi 46 katika msimamo wa ligi huku Simba wakiongoza kwa idadi ya mabao ya kufunga ambayo ni 49 huku watani wao wakiwa na 38.
Simba leo inatarajiwa kusafiri kwenda Misri kuwafuata Al Masry watakaovaana Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Port Said unaoingiza mashabiki 17,988.
Djuma alisema hivi karibuni walikutana na kufanya kikao na wachezaji wao na kikubwa waliwasisitiza kusahau matokeo ya watani wao Yanga katika ligi na badala yake kuelekeza akili zao mchezo dhidi ya Al Masry.
=============================================
Kikosi cha Simba kinataraji kusafiri jioni ya leo kuelekea Misri, kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya Al Masry SC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Wafuatao ndiyo watakuwa kwenye msafara huo
1. Said Mohamed Nduda
2. Aishi Manula
3. Shomari Kapombe
4-Mohamed Hussein
5. Asante Kwasi
6. Juuko Murushid
7. Yussuf Mlipili
8. Erasto Nyoni
9. Paul Bukaba
10. Jonas Mkude
11. James Kotei
12. Said Ndemla
13. Muzamiru Yassin
14-Mwinyi Kazimoto
15. Shiza Kichuya
16. John Bocco
17. Emmanuel Okwi
18. Nicholaus Gyan
19. Laudit Mavugo
20. Juma Luizio
Kocha Mkuu - Pierre Lechantre
Kocha Msaidizi - Masoud Djuma
Kocha wa Viungo - Mohammed Aymen
kocha wa Makipa - Muharami Mohammed
Docta wa Timu - Yassin Gembe
Meneja wa Timu - Richard Robert
Mtunza Vifaa - Yassin Mtambo
KOCHA WA STAND AISIFIA TFF YA KARIA KWA KUSEMA HAYA
Kocha
Msaidizi wa Stand United, Athuma Bilal 'Bilo', ametoa mtazamo wake
kuhusiana na mwenendo wa Shirikisho la Soka nchini namna unavyoenda
tangu uingie madarakani Agosti 2017.
Bilo
ameeleza kuwa TFF ya sasa iliyo chini ya Rais Wallace Karia,
imejitahidi kufanya marekebisho kadhaa ambayo hayakuwa yanaonekana
kipindi cha uongozi uliopita.
Kocha
amesema wakati wa uongozi uliopita ilikuwa ni ngumu kwa timu nyingi
kwenye ligi kupata matokeo au pointi tatu halali kama ambavyo imekuwa
hivi sasa.
Bilo
ambaye kikosi cha Stand United kipo katika nafasi ya 11 kwenye msimamo
wa ligi, ametoa sifa pia kwa waamuzi walio chini ya watala wa awamu hii
kuwa wamekuwa wakijitahidi ukiachana na kipindi cha nyuma.
Licha
ya hayo, Bilo ameliomba Shirikisho kuendelea kuboresha mabadiliko haswa
kwa waamuzi ambao wengi wamekuwa wakiharibu taswira ya timu kupata
matokeo halali, pia kudhorotesha mpira wa Tanzania.
Yanga timu pekee iliyoshinda mechi nyingi mfululizo VPL hadi sasa
Kwa mujibu wa takwimu za michezo ya ligi kuu Tanzania bara (VPL) Yanga ndiyo timu pekee ambayo imeshinda mechi nyingi mfululizo kati ya timu tatu za juu zinazowania ubingwa wa ligi hadi sasa.
Yanga imeshinda mechi nane zilizopita mfululizo na kujikusanyia alama 24. Tangu Januari 21, 2018 iliposhinda 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting, mabingwa hao mara tatu mfululizo wa VPL wameendelea kushinda mechi zao za ligi hadi Machi 12 walipoishinda Stand United kwa magoli 3-1.
Mara ya mwisho Yanga kushindwa kupata ushindi kwenye mchezo wa ligi ilikuwa Januar 17, 2018 Mwadui ilipowalazimisha suluhu kwenye uwanja wa Uhuru, Dar.
21/01/2018 Ruvu Shooting 0-1 Yanga
27/01/2018 Azam 1-2 Yanga
03/02/2018 Lipuli 0-2 Yanga
06/02/2018 Yanga 4-0 Njombe Mji
14/02/2018 Yanga 4-1 Majimaji
18/02/2018 Ndanda 1-2 Yanga
09/03/2018 Yanga 3-0 Kager Sugar
12/03/2018 Yanga 3-1 Stand United
Simba inafuata nyuma ya yanga, wekundu wa msimbazi wameshinda mechi tano mfululizo kati ya nane lakini imeshinda mechi sita kwa ujumla kati ya hizo nane (kuna mechi ambayo walishinda lakini haikuwa kwenye mfululizo wa mechi za ushindi) walijikuta wakilazimishwa sare mbili na timu za shinyanga (mwadui 2-2 simba, simba 3-3 stand united).
Simba bado inashikilia rekodi ya klabu ambayo bado haijapoteza mchezo hata mmoja wa ligi baada ya kucheza mechi 20.
Vinara hao wa ligi hadi sasa wamefanikiwa kutengeneza alama 20 kati ya 24 ambazo walikuwa wakiziwania katika michezo nane iliyopita.
18/01/2018 Simba 4-0 Singida United
22/01/2018 Kagera Sugar 0-2 Simba
28/01/2018 Simba 4-0 Majimaji
04/02/2018 Ruvu Shooting 0-3 Simba
07/02/2018 Simba 1-0 Azam
15/02/2018 Mwadui 2-2 Simba
26/02/2018 Simba 5-0 Mbao
02/03/2018 Simba 3-3 Stand United
Azam bado ipo kwenye mbio za ubingwa wa ligi licha ya mwendo wake wa kusuasua, katika mechi nane ziliopita imeshinda mechi tatu tu mfululizo, lakini katika hizo mechi nane wameshinda michezo minne wamepoteza mechi mbili na kutoka sare michezo miwili.
Katika michezo nane iliyopita, azam wamepata jumla ya pointi 14.
27/01/2018 Azam 1-2 Yanga
03/02/2018 Azam 3-1 Ndanda
07/02/2018 Simba 1-0 Azam
11/02/2018 Kagera Sugar 1-1 Azam
16/02/2018 Lipuli 0-0 Azam
03/03/2018 Azam 1-0 Singida United
08/03/2018 Azam 1-0 Mwadui
11/03/2018 Azam 2-1 Mbao
KLABU BINGWA BARANI ULAYA,SEVILLA JE WANAVUNJA UBABE WA MANCHESTER UNITED.
Rekodi zinaonesha kwamba asilimia 70 ya timu ambazo zilitoka suluhu ya bila kufungana ugenini katika mechi ya kwanza, zilifanikiwa kufudhu kwa hatua inayofuata katika michuano ya Champions League.
Kuna njaa sana ya mabao kwa Manchester United dhidi ya vilabu vya kutoka Hispania kwani katika michezo 15 kati ya United na timu za Hispania, United wameshindwa kufunga bao zaidi ya moja, wakifunga 7 katika michezo yote.
Jose Mourinho katika michezo yake 69 ya Champions League amepoteza michezo saba tu nyumbani, na katika michezo hiyo saba aliyopoteza, michezo 5 ni dhidi ya timu kutoka Hispania.
Katika hatua kama hii Manchester United wamepoteza mchezo mmoja tu dhidi ya timu kutoka Hispania katika mechi zao 9 zilizopita na ilikuwa mchezo wao vs Real Madrid msimu wa 2012/2013.
Ni Barcelona tu (mabao 2) ndio ambao wameruhusu nyavu zao kuguswa mara chache zaidi katika msimu huu wa Champions League kuliko Manchester United ambao wameruhusu mabao 3.
Sevilla wanaelekea katika mchezo huu wakiwa na mkosi nchini Uingereza kwani katika michezo yao minne nchini humo hawajawahi kupata ushindi, wakiwa wametoka suluhu mara tatu na kusuluhu mara moja.
TSHISHIMBI ATANGAZWA KUWA MCHEZAJI BORA LIGI KUU MWEZI FEBRUARI
Shirikisho
la Mpira wa Miguu (TFF) kupitia Bodi ya Ligi, limemtangaza Mchezaji,
Kiungo wa Yanga, Papy Kabamba Tshishimbi, kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu
Bara kwa mwezi Februari.
Tshishimbi ametwaa tuzo hiyo baada ya kuisaidia timu yake kuvuna alama 12 huku akifunga mabao matatu na akitengeneza moja.
Mechi
ambazo Tshishimbi alihusika kwenye ushindi katika mwezi Februari ni
dhidi ya Majimaji, Njombe Mji, Ndanda na Lipuli ya Iringa.
Pius
Buswita (Young African) na Emmanuel Okwi (Simba SC) ni wachezaji ambao
waliokuwa kwenye kinyang'anyiro cha tuzo hiyo kwa mwezi huu wa pili.
Tshishimbi ambaye ni mshindi wa tuzo hii, atazawadiwa kitita cha milioni moja sambamba na king'amuzi cha Azam TV.
WANAOISUBIRI SIMBA WALAZIMISHWA SULUHU KWAO KWENYE LIGI
Klabu ya Al Masry imelazimishwa suluhu ya 0-0 dhidi ya El Entag El Harby katika mchezo wa Ligi Kuu Misri uliopigwa jana.
Al Masry wamelazimishwa suluhu hiyo wakiwa wanajiandaa kuwakabili vinara wa Ligi Kuu Bara, Simba SC, Jumamosi ya wiki hii kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Africa.
Kuelekea mechi hiyo, Al Masry sasa ipo nafasi ya 4 katika msimamo wa Ligi Kuu nchini humo ikiwa na pointi 49 wakiwa wamecheza michezo 26.
Mechi yao dhidi ya Simba itafanyika Machi 17 2018 kwenye Uwanja wa Port Said Jumamosi ya wiki hii.
KUKWEPA KUONDOLEWA KIBARUANI, CARRAGHER AOMBA RADHI BAADA YA KUMTEMEA MATE SHABIKI WA MANCHESTER
Mkongwe aliyewahi kuichezea Liverpool, Jammie Carragher, ameomba radhi kutokana na kitendo cha kumtemea mate binti mwenye miaka 14 ambaye ni shabiki wa Manchester United.
Carragher alionekana akimtemea mate binti huyo aliyekuwa kwenye gari na baba yake, ikiwa ni mapema baada ya mechi iliyowakutanisha Manchester United na Liverpool Jumamosi iliyopita.
Binti huyo alimtania Carragher kuhusiana na matokeo ambayo Liverpool alifungwa 2-1, jambo lililosababisha mkongwe huyo kupandwa na hasira.
Carragher ambaye ni Mchambuzi kwenye kituo cha Sky Sports TV, alimpigia msichana huyo Jumapili ya jana kumuomba msamaha kwa kitendo alichokifanya na binti huyo alipokea msamaha wake.
Kwa mujibu wa Sky Sports TV, Msemaji wa Chombo hicho amesema kitendo alichokifanya Carragher si cha kuchukuliwa kawaida, hivyo watakutana naye na ikiwezekana watachukua hatua dhidi yake.
MMILIKI WA TIMU YA LIGI KUU UGIRIKI AINGIA NA BASTOLA UWANJANI AMFYATUE MWAMUZI ALIYEKATAA BAO LA TIMU YAKE
Mechi
ya Ligi Kuu nchini Ugiriki imesitishwa ghafla baada ya mmiliki wa timu
moja iliyokuwa inacheza kuingia na bastola uwanjani akitaka kumfyatulia
mwamuzi.
Mechi
hiyo kati ya Paok Salonika dhidi ya AEK Athens ilivunjika dakika za
nyongeza baada ya Paok kupata bao dakika za nyongeza lililofungwa na
Ferndando Varela.
Wakati
huo Paok walikuwa nyuma kwa bao 1-0 na hilo lilikuwa bao la
kusawazisha. Lakini mwamuzi alisema halikuwa sahihi sababu ilikuwa ni
offside.
Mmiliki
wa Paok, Ivan Savvidis ambaye ni mfanyabiashara mkubwa nchini Ugiriki
aliamua kuingia uwanjani akiwa na bastola yake tayari kufyatua.
Hata
hivyo zilifanyika juhudi kubwa kumuwahi na kumzuia aisitimize
alichotaka kukifanya. Walinzi wake ndiyo waliofanya kazi hiyo
kuhakikisha wanamdhibiti.
Mashabiki walitakiwa kutoka na kwenda makwao mara tu baada ya mechi hiyo kutoendelea.
Hata hivyo kulikuwa na mkanganyiko kwamba mwamuzi Giorgos Kominis alilikubali bao hilo lakini kukawa na hali ya kutoeleweka.
AEK walikuwa kileleni kwa tofauti ya pointi 3 dhidi ya Paok jambo lilimfanya mmiliki huyo kuona kama wanaonewa.
LIGI YA MKOA WA DODOMA YAENDELEA KUSHIKA KASI
Baada ya hapo jana Ligi ya mkoa wa dodoma kumaliza hatua ya kwanza ya makundi kwa vituo vya dodoma mjini na kituo cha mpwapwa.
ligi
hiyo inaingia katika hatua nyingine ya sita bora ambayo inatarajia
kuanza kutimua vumbi mwezi huu tarehe 14 ,huku pia dirisha la usajili
likiwa limefunguliwa kwa vilabu ambavyo vimeingia hatua ya sita bora
Ni WATUMISHI,AREA D,GURRENS,SHELI AJAX,GWASSA.
Katibu wa chama cha soka mkoani dodoma akizungumzia hayo baada ya hatua ya awali kukamilika hapo jana nini kinafuata katika ligi hiyo.
Amesema
kuwa ligi ya mkoa wa dodoma hatua ya sita bora inatarajia kuendelea
siku ya jumatano tarehe 14 ambapo kwa sasa vilabu vimepewa nafasi ya
kufanya usajili wa wachezaji
Kikosi
cha Simba kimeonesha kweli kimedhamiria kuibuka na ushindi dhidi ya Al
Masry SC katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kesho.
Katika
hali isiyo ya kawaida, kikosi hicho kilifanya mazoezi kuanzia majira ya
saa moja mpaka mbili usiku wa jana kwenye uwanja wa Boko Vetarani, Dar
es Salaam.
Taarifa zinaeleza kuwa wachezaji wapo katika morali nzuri kuelekea mchezo huo utakaopigwa majira ya saa 12 jioni.
Aidha wachezaji Emmanuel Okwi, John Bocco na Haruna Niyonzima wote walijumuika na wenzao kujifua kuelekea mechi hiyo kubwa.
Simba watafanya mazoezi ya mwisho leo kabla ya kuwavaa Al Masry jioni ya kesho.
MAN UNITED IMERUDI MAFASI YA PILI
Manchester
United imerudi kwenye nafasi yake ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu
Uingereza baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Crystal
Palace.
Mchezo
huo ambao ulikuwa na matokeo hasi kwa Manchester United katika kipindi
cha kwanza, ulimalizika huku Palace akiwa na bao moja lililofungwa na
Townsend dakika ya 11.
Mpaka mapumziko Palace alikuwa mbele kwa bao 1-0.
Kipindi
cha pili kilipoanz, Palace walifunga bao la pili na kuufanya mchezo uwe
mgumu kwa United baada ya van Aanholt kufunga bao dakika ya 48 ya
mchezo.
United
walirudi kwa kasi mnamo dakika ya 55 Smalling alifunga, baadaye dakika
ya 76 Lukaku naye akacheka na nyavu na mchezo kuwa sare ya 2-2.
Dakika za mwisho kabisa ikiwa imeongezwa moja mchezo umalizike, Matic alipigilia msumari wa mwisho na kufanya matokeo yawe 2-3.
United sasa imerudi tena nafasi ya pili kwa kufikisha alama 62, juu ya Liverpool iliyo na 60.
===========================================
NEYMAR MTABA WAKE NA KAMPUNI YA NIKE WAVUJA
Yuko majeruhi na sasa inadaiwa kwamba Neymar itabidi afanyiwe operesheni ambayo inaweza kumuweka nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi mitatu hali ambayo inaweka mashakani kiwango chake.
Lakini wakati Neymar akiwa majeruhi, mkataba wake na kampuni ya vifaa vya michezo ya Nike umevuja, mkataba wa Neymar na Nike unaonesha kila kitu atakachopewa katika soka lake kuanzia sasa.
Mwanzo Nike walikuwa wakilipana kiasi cha €40m kwa mwaka na sasa Nike wako tayari kutoa $1million kwa Neymar kama atachukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia (Ballon D’or) mwakani kama Bonus.
Kiasi hiki ambacho Neymar atapewa na Nike kama akichukua Ballon D’Or kitakuwa kikiongezeka kwa 100% kila mwaka atakayobeba tuzo hiyo na hii ina maana kwamba hadi 2022 anaweza pokea hadi bonus $4million.
Nike hawajaishia hapo kwani bado wana mpunga mrefu wameutenga kwa ajili ya mchezaji huyo wa Kibrazil katika michuano ya kombe la dunia inayotarajiwa kuanza hivi karibuni nchini Urusi.
Endapo Neymar atabeba kombe la dunia Nike watamkabidhi kiasi cha $50,000 na kama nyota huyo atamaliza michuano hiyo mikubwa zaidi duniani akiwa kama mfungaji bora wa michuano hiyo atachukua $200,000.
MAN CITY MICHEZI 4 ZAKUWAPA UBINGWA
Klabu ya Manchester city jana Jumapili wakiwa uwanja wao wa nyumbani wa Etihad walifanikiwa kuchomoza na ushidi wa bao 1-0 dhidi ya Chelsea bao lilifungwa na Bernardo Silva Dakika ya 46 kipindi cha pili cha mchezo.
Ushindi huo Manchester City umezidi kuwaimarisha kileleni mwa ligi kuu ya England kwa kujikusanyia alama 78 wakifuatiwa na klabu za Liverpool alama 60, Manchester United alama 59,Tottenham Hotspurs alama 58, Tottenham alama 53,huku klabu za West Bromwich Albion,Stoke city na Crystal Palace zikiendelea kushikiria nafasi za mwisho.
Katika mchezo mwingine Brighton wakiwa ni wenyeji wa Arsenal walifanikiwa kupata alama tatu kwa ushindi wa mabao 2-1, Magoli ya Brighton yakifungwa na Lewis Dunk pamoja na Glenn Murray huku bao la Arsenal bao lao la kufutia machozi likifungwa na Pierre-Emerick Aubameyang.
Ligi hiyo ya England inaratarajia kuendelea tena leo jumatatu kwa mchezo mmoja ambapo Crystal Palace wanawakaribisha Manchester United.
YANGA WAJIANDAA KWA ASILIMIA 100 KUWAVAA ROLLER
Katibu Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa amewaondoa hofu mashabiki wa Yanga akiwataka mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanjani kesho.
Mkwasa alisema shabiki ni mchezaji wa 12, hivyo kujitokeza kwa wingi kutaongeza kutoa hamasa kwa wachezaji kupambana.
Aliongeza kuwa, kikosi chao kipo fiti kwa ajili ya mchezo huo, amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi.
KIINGILIO cha chini katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika baina ya Yanga na Township Rollers ya Botswana Jumanne kitakuwa ni Sh. 5,000.
Taarifa ya Yanga leo imesema kwamba viingilio vingine vitakuwa ni Sh. 20,000 kwa VIP A na Sh. 15,000 kwa VIP B na C.
Mchezo huo unatarajiwa kufanyika Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam kuanzia Saa 10:30 na timu hizo zitarudiana siku 10 baadaye nchini Botswana.
Yanga itakabiliana na Township Rollers ya Botswana katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika katika uwanja wa taifa, Dar es Salaam, saa 10 kamili jioni.
Upande wa township rollers
Kuelekea mechi ya kesho kati ya Yanga dhidi ya Township Rollers ya Botswana katika mchezo wa Ligi Ya Mabingwa Afrika, Kocha Nikola Kavazovic, amesema analijua soka la Afrika.
Kavazovic amesema amekuwa akilifuatilia vizuri soka la Afrika, na timu yake ipo tayari kupambana na wapinzani katika mchezo wa kesho.
Licha ya kulijua soka la Afrika, Kavazovic, amesema amekuwa akiifuatilia pia Yanga katika michezo mbalimbali ya kimataifa iliyocheza, huku akieleza ameshaitazama ikicheza miwili ya nyumbani na miwili ya ugenini.
==============================================
WACHEZAJI wawili wa Azam FC, Nahodha Himid Mao ‘Ninja’ na mshambuliaji Wazir Junior, wamerejea rasmi mazoezini jana baada ya kukosekana dimbani kwa muda mrefu wakiuguza majeraha yanayowakabili.
Himid alikuwa akisumbuliwa na maumivu chini ya goti la mguu wake wa kulia huku Junior akikabiliana na tatizo kwenye kifundo chake cha mguu wa kulia, na tayari nyota hao wameanza kupata nafuu na sasa wanamalizia programu ya mazoezi mepesi kabla ya kuruhusiwa kurejea rasmi katika ushindani.
Nyota hao wamerejea wakati kikosi cha Mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA Kagame Cup) kikijiandaa na mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) dhidi ya Singida United, utakaofanyika Uwanja wa Azam Complex Jumamosi hii saa 1.00 usiku.
Junior anayetakiwa kufanya programu hiyo ya mazoezi mepesi kwa muda wa wiki moja, alisema anamshukuru Mungu kurejea tena dimbani huku akikiri kuwa ‘amemiss’ kucheza mpira.
“Kikubwa
ni kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kurudi tena na nitaendelea kujituma
kama ilivyokuwa awali kutokana na majeruhi haya ndo ilikuwa hivyo lakini
tutapambana kama ilivyokuwa mwanzo, nimeumiss sana mpira nimemiss sana
kucheza mpira na kuonyesha vile mashabiki wanataka.
“Lakini
naamini kwa rehema za mwenyezi Mungu tutakaporejea tena basi mashabiki
watafurahia vile walivyokuwa wakivisubiria,” alisema Junior
Mchezo
huo unatarajia kuwa mkali na wa aina yake kutokana na ushindani wa timu
hizo uliokuwa kwa siku za hivi karibuni, tokea Singida United irejee
Ligi Kuu msimu huu, ambapo katika mtanange wa mzunguko wa kwanza
uliofanyika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, timu hizo zilitoka sare ya bao
1-1.
YANGA KUVUNJA MWIKO? AU NDANDA KUENDELEZA UNDAVA?
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja tu, mabingwa watetezi, Yanga SC wakiwa wageni wa Ndanda FC Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Huo ni mchezo wa kiporo wa mzunguko wa 19, ambao Yanga ilishindwa kuucheza kutokana na kukabiliwa na mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Saint Louis Suns United ya Shelisheli.
Na baada ya kuvuka Raundi ya Awali kwa ushindi wa jumla wa 2-1, ikishinda 1-0 nyumbani na sare ya 1-1 ugenini, Yanga inakuja kumalizia kiporo chake kabla ya kwenda kucheza mechi ya Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Township Rollers ya Botswana.
Lakini Yanga itateremka Uwanja wa Nangwanda jioni ya leo ikiwa kumbukumbu ya kutoshinda mechi nyumbani kwa Ndanda kati ya nne zilizotangulia, wakifungwa mbili na sare mbili.
Kwa ujumla, katika Ligi Kuu Yanga imekutana na Ndanda mara nane tangu hiyo ipande msimu wa 2014/2015 – huku mabingwa hao watetezi, wakishinda mechi tatu, kufungwa mbili na sare tatu.
Yanga itajaribu kusaka ushindi wa kwanza leo Uwanja wa Nangwanda ikiwa inabakiliwa na wimbi la majeruhi na matatizo mengi ndani ya timu.
RAIS WA FIFA ALIVYOPOKELEWA NA NGOMA ZA ASILI KABLA YA KUFUNGUA MKUTANO
Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino, amepokelewa na ngoma za kiasili kutoka kwa kabila la Wamasai, ambao walimbatana na zawadi mbalimbali za kiasili.
Infantino
alipokea zawadi hizo leo mapema, kabla ya kufungua mkutano wa FIFA
Excutive Summit, katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam.
Infantino
amewasili hapa akiwa na viongozi wengine mbalimbali, ikiwemo Rais wa
CAF, Mr. Ahmad, kwa ajili ya mkutano wa mwaka wa FIFA unaoanza leo
February 22.
Ujio
wa Rais huyo ni maalum kwa ajili ya majadiliano kuhusu Soka la
Wanawake, Vijana, Mipango ya kukuza soka kwa nchi za Afrika, pamoja na
kusaidia vilabu kujiendeleza kisoka kiujumla.
Infantino ataondoka nchini mara tu baada ya mkutano huo kumalizika.
Tazama hapa namna alivyopokelewa na kabila la Wamasai waliombatanisha zawadi mbalimbali kwake.
ALLIANCE GIRLS:TUNAOMBA TFF WATAZAME RATIBA KWA UPANDE WETU
Wawakilishi wa kanda ya ziwa kunako Ligi soka wanawake nchini Tanzania kutoka jijini Mwanza Alliance Girls wamesema kuwa wamejipanga vilivyo kwenda kufanya kweli kunako ligi soka ya wanawake hatua ya nane bora ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi tarehe 24 mwezi huu
Hayo yamesemwa na kocha wa klabu hiyo Ezekiel Chobanga wakatia akizungumza na michezo ya dodoma mapema leo Ambapo amesema wamejipanga kwenda kufanya vema katika mchezo wao wa kwanza jijini dar es salaam.
Amesema licha ya kutarajia kuanza kushiriki ligi hiyo lakini bado changamoto kubwa ambayo inawakabili ni Ratiba kuwabana kutoka na kushiriki mechi ya kwanza dar es salaam ,Mwanza na hatimaye ten Dodoma
Naye Nahodha wa timu hiyo ameelezea namna walivyojipanga yeye pamoja na wachezaji wenzake kuelekea nane bora ya ligi ya soka upande wa wanawake ambayo inatarajia kuanza mwezi wa pili tarehe 24 .
Kwa upande mwingine Amesema kuwa jamii wamekuwa wakitoa ushirikiano kwakuhakikisha watoto wa kike wanashiriki katika mchezo wa mpira wa miguu.
Na Selemani Juma Kodima
DOREFA DODOMA: LIGI YA MKOA WA DODOMA KUANZA FEBRUARY 23.
Ligi ya mkoa
wa dodoma inatarajia kuanza kutimua vumbi siku ya ijumaa feb 24 baada ya ratiba
ya ligi hiyo kutoka rasmi hapo jana ambapo mechi nne zitaanza kuchezwa katika
viwanja vya ccm jamhuri na ccm mgambo wilayani mpwapwa.
Ratiba hiyo
inaoneshwa kuwa Timu kutoka wilayan kondoa ambapo wapo kituo cha dodoma mjini
watacheza saa nane kamili mchana dhidi ya timu ya Dom city kutoka zuzu hku
jioni kukiwa na mchezo baina ya Derby ya Chamwino ya zamani Ila kwa sasa kila
timu ipo kata yake ,Gwasa nato kutoka chang'ombe wakicheza na Sheli Fc matajiri
kutoka chamwino katika mchezo wa jioni tarehe 23.
Wakati katika
kituo cha Mpwapwa kutakuwa na michezo miwili ambayo itapingwa katika dimba la
CCM mgambo kwa muda husika wa saa nane kwa mchezo wa kwanza na saa kumi kamili
jioni kwa mchezo wa jioni.
Ligi ya mkoa
wa dodoma ilitarajia kuanza mwezi wa
kwanza lakini kutoka na vilabu shiriki kushindwa kutekeleza kwa wakati vigezo
vya chama cha soka dodoma Pamoja na Tff imepelekea kuchelewa kwa ligi hiyo.
Na Selemani Juma Kodima
Conte: Tutailaza Barcelona mechi ya marudio Ligi ya Mabingwa Ulaya UEFA
Mkufunzi Antonio Conte amesema kuwa Chelsea "itajaribu kufanya kitu cha kipekee'' na kuitoa Barcelona katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya sare 1-1 katika awamu ya kwanza
Willian aliiweka kifua mbele The Blues lakini Lionel Messi alisawazisha dakika 15 kabla ya mechi kukamilika baada ya makosa ya Andreas Christensen katika mechi ya kufuzu katika robo fainali ya kombe hilo.
Barcelona ambayo iko pointi saba mbele kileleni La Liga haikutekeleza mashambulizi yoyote makali hadi waliposawazisha.
''Tulikuwa tunakaribia kuwafunga," alisema mkufunzi huyo wa Chelsea. ''Tulifanya kosa moja, ni aibu na tumevunjwa moyo na matokeo''.
Simba imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gendamarie na kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho kwa idadi ya mabao 5-0.
Katika mechi ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Simba ilishinda kwa mabao 4-0.
Bao la leo la Simba lilifungwa na Emmanuel Okwi, Simba ikiwa imekianza kipindi cha pili kwa kasi kubwa.
Mechi hiyo ilikwenda mapumziko kwa sare ya bila bao huku Gendamarie wakipoteza nafasi moja ya kufunga na Simba wakipoteza tatu ikiwemo ya Okwi aliyekuwa nahodha katika mchezo wa leo.
HATUA ya 16 Bora michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) inatarajiwa kuanza kesho
HATUA ya 16 Bora michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) inatarajiwa kuanza kesho kwa mchezo mmoja tu kufanyika Uwanja wa Saba Saba mjini baina ya wenyeji, Njombe Mji FC na Mbao FC ya Mwanza,utakaoanza Saa 10:00.
Mechi
nyingine za Kombe la Shirikisho la Azam zitaendelea Jumamosi Februari
24, wakati Singida United watakapowakaribisha Polisi Tanzania kwenye
Uwanja wa Namfua saa 10 jioni na KMC watawaalika Azam FC saa 1 usiku
Azam Complex
Jumapili
Februari 25, 2018 Buseresere watakuwa uwanja wa Nyamagana Mwanza saa 8
mchana kucheza dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro, Majimaji FC ya Ruvuma
watakuwa nyumbani kwenye uwanja wa Majimaji kuwakaribisha Young Africans
ya Dar es Salaam saa 10 jioni wakati Ndanda FC watakuwa ugenini kucheza
na JKT Tanzania saa 1 usiku Azam Complex Chamazi.
Jumatatu
Februari 26, 2018 kutachezwa mechi mbili Kiluvya United dhidi ya
Tanzania Prisons saa 8 mchana Uwanja wa Mabatini na Stand United
watawaalika Dodoma FC saa 10 jioni uwanja wa Kambarage.
CONTE: NI NGUMU KUMZUIA MESSI
Kocha wa Chelsea, Antonio Conte, ameweka wazi kuelekea mchezo wa kwanza katika hatua ya 16 bora dhidi ya FC. Barcelona katika UEFA Champions League utakuwa si rahisi.
Conte ameeleza kukutana na timu kama Barcelona ambayo ipo juu ya msimamo mwa Ligi huku ikiwa haijapoteza hata mchezo mmoja inabidi kazi ya ziada ifanyike.
Mbali na hilo ameongeza pia kwa kusema kuwa amekuwa anashindwa kupata usingizi kufikiria mbinu zipi na mipango gani ifanyike ili waweze kuizuia Barcelona leo huku akiongeza kwa kumtaja Messi kuwa ni ngumu kumzuia.
Mara ya mwisho Chelsea na Barcelona kukutana ilikuwa April 2012 ambapo Chelsea iliibuka na ushindi wa mabao 3-2 (On Aggregate).
======================================================
Kenya yamsaka kocha mpya wa Harambee Stars baada ya Paul Put kujiuzulu
Kenya inamsaka mkufunzi mpya wa timu yake ya taifa baada ya kocha Paul Put kujiuzulu miezi mitatu baada ya kuzinduliwa.
Hii ilithibitishwa Jumatatu jioni na taarifa iliotolewa na shirikisho la soka nchini humo FKF kupitia meneja wa mawasiliano na uhusiano mwema Barry Otieno ambaye alielezea kwamba mkufunzi huyo alijiuzulu kutokana na matatizo ya kibinafsi huku Stanley Okumbi akichukua mahala pake kwa muda.
''Shirikisho la soka la Football Kenya lingependa kuwaambia mashabiki wa soka nchini Kenya kwamba bwana Pual Put amejiuzulu rasmi kama mkufunzi wa timu ya taifa kutokana na maswala ya kibinafsi.
''Hatahivyo kujiuzulu kwa kocha huyo ni pigo katika harakati za timu ya taifa kuelekea katika kufuzu mashindano ya AFCON 2019 kwa kuwa alikuwa kiungo muhimu cha timu''.
MBUNGE WA DODOMA MJINI AENDELEA KUHIMIZA MICHEZO ATOA JEZI KWA VILABU
Kuelekea mshikemshike wa ligi ya mkoa wa dodoma ngazi ya taifa, Naibu Waziri, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde ambaye pia Mbunge wa dodoma Mjini Antony Mavunde katika kuongeza hamasa katika ligi hiyo leo amekabidhi jezi kwa vilabu vinavyoshiriki ligi hiyo kutoka manispaa ya dodoma.
Mh Mavunde amesema kuwa katika kuongeza hamasa katika mchezo wa mpira wa miguu imemfanya kushiriki kwa kutoa jezi kwa timu za manispaa ya dodoma kuelekea ligi ya mkoa ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi Feb 21 mwaka huu.
Aidha ametoa pongezi kwa timu ya AREA C pamoja na Klabu ya DFC kwa juhudi zao katika medani ya soka kupitia ngazi za mashindano ambayo wameshiriki kwa msimu wa 2018/2019 .
Kwa upande wa vilabu ambavyo vimekabidhi jezi na mbunge huyo wametoa shukrani zao kupitia kwa moja ya viongozi wa timu ya sheli fc bw Mohamed abdalah ambaye amesema kuwa kutoka na uwepo changamoto hiyo ambayo mbunge ameitazama na kuwasaidia basi wamejipanga kulipa fadhila kwa kuhakikisha ubingwa wa mkoa unabaki dodoma mjini
Na Selemani Juma Kodima
LIGI YA MKOA WA DODOMA INATALAJIWA KUANZA TAREHE 24 MWEZI WA PILI
Dodoma
Na ligi ya mkoa wa dodoma inatarajia kuanza kutimua vumbi tarehe 24 mwezi wa pili mwaka huu kwa mfumo wa makundi mawili.
Hayo yamesemwa na katibu wa chama cha soka mkoani dodoma Dorefa Hamis kisoi wakati akielezea ligi ya mkoa wa dodoma, na namna chama kimefikia hatua gani katika maandalizi ya ligi hiyo
Hamisi kisoi amesema kuwa kutokana na ligi hiyo kuwa na Muda mchache wamejipanga kuhakikisha wanaisimamia vizuri ili kupata bingwa ambaye ataweza kwenda kuwakilisha mkoa wa dodoma kunako mabingwa wa mikoa
Na Selemani Juma Kodima
KLABU YA SOKA YA WANAWAKE YA MKOA WA DODOMA BAOBAO FC IMEWAOMBA WAKAZI WA MKOA WA DODOMA KUENDELEA KUISAIDIA TIMU HIYOKlabu ya soka ya wanawake ya mkoa wa dodoma Baobao fc imewaomba wakazi wa mkoa wa dodoma kuendelea kuisupport timu hiyo ambayo inashiriki ligi kuu hatua ya nane bora kwa mahitaji mbalimbali ikli iweze kufanya vema katika ligi hiyo
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa klabu hiyo Inocensi Massawe wakati akizungumza na sport bomba juu ya maandalizi yao na namna walivyojipanga katika kujianda na ligi hiyo ambayo inatarajia kuanza feb 24 mwaka ambapo baobao queen wanaanzia nyumbani wakicheza na klabu ya mlandizi ya mkoani pwani https://www.hulkshare.com/xsjmi4g7usqo
Na Selemani Juma Kodima
YAKUBU MOHAMMED ASEMA ATAENDELEZA MOTO KATIKA MICHEZO YA LIGI
Na Dodoma Fm
BAADA ya kushinda tuzo Mchezaji Bora wa Mwezi
Agosti wa Azam FC, beki Mghana Yakubu Mohammed amepania kufanya mambo makubwa
zaidi kuisaidia timu hiyo.
Yakubu ametwaa tuzo hiyo inayojulikana kama ‘NMB
Player of the Month’ ikidhaminiwa na wadhamini wakuu wa timu hiyo Benki ya NMB,
na anakuwa mchezaji wa kwanza wa Azam FC kuitwaa ikiwa imeanzishwa msimu huu.
Kwa upande wa timu ya vijana ya Azam FC (Azam FC
U-20) tuzo hiyo imekwenda kwa kiungo Twaha Ahmed, ambayo inadhaminiwa na
wadhamini namba mbili wa timu hiyo Maji safi ya Uhai Drinking Water ikijulikana
kama ‘Uhai Player of the Month’.
Tuzo hizo za kwanza za Azam FC, zilitolewa na
mgeni rasmi kwenye mchezo wetu wa jana dhidi ya Lipuli, Rais wa Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia.
Akizungumza jana mjini Dar es Salaam, Yakubu
aliishukuru Azam FC kwa kuanzisha tuzo hiyo akidai inaongeza ushindani kikosini
pamoja na kujenga wasifu wa wachezaji (CV).
MILIONI 47 KUIPANDISHA DARAJA TIMU YA AREA C
Na Dodoma Fm
Timu ya Soka ya AREA C
ya mkoani dodoma ambayo itashiriki ligi daraja la pili katika msimu wa 2017/2018 imetoa
shukrani kwa serikali ya mkoa wa dodoma
baada ya kuwa nao bega kwa bega katika hatua zote za michezo yao ya ligi ya mabingwa wa
mikoa iliyomalizika hivi karibuni.
Pongezi hizo na shukrani zimetolewa na Uongozi
wa Timu ya Area C walipokuta na Mkuu wa mkoa wa dodoma Mh
Jordani Rugimbana pamoja na viongozi wengine wa mkoa ambapo wamekabidhi nishani
ya shukrani kwa kila ambacho wamewasaidia
kuweza kupanda daraja .
Licha ya shukrani hizo ,timu hiyo imewasilisha bajeti yao kuu mbele ya
mkuu wa mkoa ambayo itawawezesha
kufanikiwa kushiriki vema ligi daraja la pili
na hatimaye kupanda daraja la kwanza kuwa Millioni 47 na Elfu 90 .
Comments
Post a Comment