Skip to main content

Serikali Haitafumbia Macho Maswala ya Adhabu Kali Mashuleni

         Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni mjini Dodoma.     


Ametoa wito juu ya Maafisa Elimu wa mikoa na Maafisa  Elimu wilaya kuwakumbusha walimu kote nchini kuzingatia muongozo wa utoaji wa adhabu shuleni chini ya kifungu namba 61 cha sheria ya elimu sura ya 353 ya sheria pamoja na kanuni zake.

Na Martha Mgaya

Serikali imetoa wito huu kufuatia kusambaa kwa video fupi katika mitandao ya kijamii iliyomuonesha mwalimu wa shule ya msingi Kakanja iliyopo Wilaya ya Kyerwa, Mkoa wa Kagera akimpiga vikali mwanafunzi wa shule hiyo.


Akizungumzia juu ya tukio hilo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alieleza kuwa vitendo kama hivyo, vimesababisha madhara mengi ikiwemo kuleta taharuki kwa jamii ,athari ya kimwili ,kiakili na msongo wa 

“Serikali haitofumbia macho na wala kukubaliana na aina hiyo ya adhabu kali. Tayari serikali imechukua hatua za kinidhamu kwa wahusika.’’ anaeleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.


Anasema serikali imekuwa ikitekeleza afua mbalimbali kuhakikisha ulinzi na usalama wa mtoto awapo kwenye mazingira yote.Licha ya kuwepo kwa mifumo hiyo kuna ukiukwaji wa sheria na taribu kwa makusudi , hivyo kusababisha madhara makubwa kwa jamii .


Pia, Waziri Majaliwa amezitaka Mamlaka za elimu nchini kuhakikisha kuwa utoaji wa adhabu shuleni unazingatia waraka namba 24 wa mwaka 2002 wa Wizara ya Elimu na Utamaduni ambao umeainisha utaratibu wa utoaji wa adhabu.


“Mwanafunzi wa kike atapewa adhabu ya viboko mkononi na mwalimu wa kike isipokuwa kama shule hiyo haina mwalimu wa kike”


“Adhabu ya viboko itakapotolewa iorodheshwe katika kitabu kilicho tengwa kwa kusudi hili ikiwa ni pamoja jina la mwanafunzi aliyepewa adhabu ,kosa alilotenda,idadi ya viboko na jina la mwalimu aliyetoa adhabu hiyo.’’ anafanua Majaliwa wakati akielezea taratibu zinazo paswa kuzingatiwa wakati wa utoaji adhabu.


Hatua zingine zilizotajwa katika muongozo ni pamoja na Mwalimu mkuu kusaini katika kitabu kila  mara adhabu hiyo inapotolewa  na endapo mwanafunzi akikataa adhabu ya viboko atasimamishwa shule.


Sambamba na hilo Waziri Majaliwa ameeleza kuwa walimu wamekuwa wakifanya kazi kubwa kuliko mapungufu machache yanayoonekana kupitia mitandao ya kijamii. Hivyo kuitaka jamii kutoyarusha matukio yanayo fanywa na baadhi ya walimu  kwenye mitandao.

“Bahati mbaya kwa jamii zetu jambo baya linasambaa zaidi kuliko jema.’’ anasema Majaliwa, “hata hivyo , licha ya mapungufu kutoka kwa baadhi ya walimu, walimu wanafanya mambo mengi makubwa malezi kwa watoto wetu ambayo pengine hayakusambaa na kuonekana. Jamii haipaswi kubeza juhudi zinazo fanywa na walimu badala yake muwatie moyo.’’


Majaliwa amesisitiza lengo siyo kuficha taarifa bali kuzuia taharuki,chuki na  uhasama ndani ya jamii, katika nyanja zote kama afya ,vyombo vya ulinzi na usalama na maeneo mengine yanayofanana na hayo.



 

Comments

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifugua kwa upasuaji na

SERIKALI IMEANZA KUANDAA KITINI CHA MASUALA YA JINSIA

                                             Serikali imeanza mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza katika kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto umekithiri sana nchini   hivyo Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo. Amesema   lengo la kuandaa kitini cha kufundishia masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii. Bi. Mboni amefafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Is