Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalaani na kukemea
matukio ya ukatili wa kijinsia hasa kwa wanawake yaliyotokea hivi karibuni
katika Mkoa wa Dodoma Pwani na Mwanza.
Wizara imepokea taarifa za ukatili kwa
wanawake hao kwa mshituko makubwa, na ina kemea vitendo hivyo vya ukatili maana
ni ukiukaji wa Haki za Msingi za binadamu.
Matukio hayo yaliyotokea Dodoma Pwani na Mwanza ni tukio la Mei 26
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) Rose Malfred (31), mkazi wa Swaswa
aliyeuawa kikatili na mumewe ambaye inadaiwa kuwa ni Mchungaji wa Kanisa la TAG
Bw. John Mwaisango, kwa kumchoma visu sehemu mbalimbali za mwili hadi kufa.
Tukio linguine
lilitokea Mei 25, mwaka huu, ambapo mwili wa Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya
Mkuranga mkoani Pwani, Rosemary Mgombela, ulikutwa umefukiwa pembeni ya nyumba
wanayoishi.
Aidha, tukio lingine
lililoripotiwa Aprili 30, mwaka huu ni la mfanyabiashara wa samaki mkazi wa
mtaa wa Mahakama wilayani Ilemela, Bw.Nicholas Light (25) ambaye alimuua mpenzi
wake, Victoria Swai (26) kwa kumnyonga na kumkaba shingo kwa wivu wa mapenzi.
Matukio hayo yote ni
kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977 inayoeleza
bayana haki ya kuishi kwa kila raia, Ibara ya 14 ya Katiba hiyo imeeleza kuwa
kila mtu ana haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake
kwa mujibu wa Sheria.
Wizara Imeasa jamii kutoa taarifa kwa vitendo vya
ukatili kwa wanawake katika jamii ili kudhibiti matukio ya ukatili hususan
mauaji ya wanawake ambayo yanafanywa na watu
NA MARIAM MATUNDU
DODOMA FM
Comments
Post a Comment