Skip to main content

WIZARA YA AFYA YAKEMEA VIKALI MATUKIO YA UKATILI YALIYOFANYIKA KARIBUNI



Image result for WIZARA YA AFYA YAKEMEA




Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalaani na kukemea matukio ya ukatili wa kijinsia hasa kwa wanawake yaliyotokea hivi karibuni katika Mkoa wa Dodoma  Pwani na Mwanza.

Wizara imepokea taarifa za ukatili kwa wanawake hao kwa mshituko makubwa, na ina kemea vitendo hivyo vya ukatili maana ni ukiukaji wa Haki za Msingi za binadamu.

Matukio hayo yaliyotokea Dodoma Pwani na Mwanza ni tukio la Mei 26 Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) Rose Malfred (31), mkazi wa Swaswa aliyeuawa kikatili na mumewe ambaye inadaiwa kuwa ni Mchungaji wa Kanisa la TAG Bw. John Mwaisango, kwa kumchoma visu sehemu mbalimbali za mwili hadi kufa.

Tukio linguine lilitokea Mei 25, mwaka huu, ambapo mwili wa Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Rosemary Mgombela, ulikutwa umefukiwa pembeni ya nyumba wanayoishi.

Aidha, tukio lingine lililoripotiwa Aprili 30, mwaka huu ni la mfanyabiashara wa samaki mkazi wa mtaa wa Mahakama wilayani Ilemela, Bw.Nicholas Light (25) ambaye alimuua mpenzi wake, Victoria Swai (26) kwa kumnyonga na kumkaba shingo kwa wivu wa mapenzi.

Matukio hayo yote ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977 inayoeleza bayana haki ya kuishi kwa kila raia, Ibara ya 14 ya Katiba hiyo imeeleza kuwa kila mtu ana haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa Sheria.

Wizara Imeasa jamii kutoa taarifa kwa vitendo vya ukatili kwa wanawake katika jamii ili kudhibiti matukio ya ukatili hususan mauaji ya wanawake ambayo yanafanywa na watu

NA MARIAM MATUNDU                                                 DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...