Skip to main content

WILAYA 93 ZAPATIWA KINGA TIBA MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE


Image result for Katibu mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mpoki Ulisubisya






Wilaya 93 nchini zilizokuwa zinahitaji kinga tiba kwa ajili ya magojwa  zimefanikiwa kutokomeza magojwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yakiwemo ya mabusha pamoja na matende.

Katibu mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mpoki Ulisubisya ameyasema hayo katika uzinduzi wa mkutano wa kujadili, kupata na kupanga utekelezaji wa mpango kazi katika kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Dk. Mpoki amesema serikali kupitia Wizara ya Afya imetoa dawa kwa watanzania wapatao milioni 21 kati ya milioni 50 na kupiga hatua kubwa katika kudhibiti magonjwa hayo hapa nchini.

Amesema mkutano huo umelenga kukutanisha wadau wa afya wa ndani na nje ya nchi wenye lengo la kutoka na mikakati ya kupambana na magojwa hayo hasa katika maeneo ya vijijini.

Nae Mratibu wa Taifa wa mpango wa kutokomeza magojwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchini Dkt. Upendo Mwingira amesema wananchi wanatakiwa kujitokeza katika mazoezi ya kupata dawa za kuzuia mabusha pamoja na matende pindi serikali itakapotangaza zoezi la utoaji wa dawa hizo.

Sambamba na hayo Mwingira amesema katika kuhakikisha magonjwa hayo yanapotea nchini wamejitahidi kuzindua kampeni ya kuwafanyia upasuaji watu wapatao 350 kisarawe Mkoani Pwani.

Na Phina Nimrod                                                                  DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...