Pamoja na elimu
inayoendelea kutolewa juu ya madhara ya ukeketaji bado kuna baadhi ya maeneo
yanaonesha kuendeleza vitendo hivyo vya kikatili kwa wanawake.
Dodoma fm
imezungumza na baadhi ya wazee wa kimila katika kijiji cha Chikopelo wilayani Bahi
ambao wameonesha kutamani kuendeleza vitendo hivyo isipokuwa wanaogopa vyombo
vya sheria.
Kutokana na imani
ya wazee hao kituo hiki kimezungumza na kaimu mganga mkuu mkoa Dodoma Mzee Nasoro
ambae amesema mwanamke aliyekeketwa anapata madhara makubwa wakati wa
kujifungua ikiwamo kupoteza damu nyingi na hata kupelekea kifo kwa mtoto.
Nae mgaguzi
msaidizi wa polisi kutoka dawati la jinsia na watoto Lovie Mhena amesema
Vitendo vya ukeketaji vimetajwa kuwa ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria
ambapo adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 jela.
Kutoka mtandao wa
wanawake Tanzania bi Sara Mwaga anasema pamoja na tafiti kuonesha dodoma
inashika nafasi ya pili katika ukeketaji lakini elimu inayotolewa na asasi za
kiraia zinazaa matunda kutokana na watu walio wengi kubadili mitazamo na kuacha
ukeketaji.
Mkoa wa Dodoma ni
wapili katika mikoa mitano inayomgoza kwa ukeketaji ikiwa na 47%huku mkoa
unaongoza ukiwa ni Manyara wenye 58% na mkoa wa Arusha ukiwa na 41%Mara ikiwa
na 32% na Singida 31%.
NA
MARIAM MATUNDU DODOMA FM
Comments
Post a Comment