Jamii imetakiwa
kufuata taratibu za kisheria katika ununuzi wa ardhi ili kuepuka migogoro ya
ardhi inayojitokeza mara nyingi miongoni mwa familia.
Rai hiyo imetolewa
na Mwanasheria wa Kujitegemea Bwana Goodluck Ludala ambapo amesema migororo
mingi ya ardhi inatokana na watu kutokufuata taratibu za kisheria za manunuzi
ambapo inaweza kupelekea mtu kupoteza haki yake .
Amesema iwapo mtu
atapata migogoro ya ardhi anatakiwa kupeleka shauri lake baraza la kata na
baada ya uamuzi kutoka mlalamikaji anapaswa kukaza hukumu katika baraza la
ardhi la wilaya jambo ambalo watu wengi huwa hawafanyi na kupoteza haki zao.
Aidha amesema
kumekuwa na baadhi ya watu wanaopuuza hukumu ya mahakama pasipo kukata rufaa ambapo
ameeleza kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria na hapo mlalamikaji anapaswa kutoa
taarifa katika mahakama iliyotoa hukumu ili hatua zaidi zichukuliwe.
Haya Yamejiri ikiwa
ni siku chache baada ya Dodoma FM kupokea kisa cha migogoro ya ardhi katika
familia ambako kulionekana kuwa na tatizo la
kupuuza amri ya mahakama.
Mariam
Matundu DODOMA FM
Crytpcurrency ethereum to bank account live instant conversion with 0% fee from the worlds most trusted website. You can sell your ether coin to receive money into your bank account in form of local cash. (:O:) feel blessed
ReplyDeleteLatest platform for web marketing and search engine marketing (SEM) and (SEO) tool. This tool provides a complete SEO skill. The mostly person uses search engine marketing for online marketing. this totally depends on latest trends in search engine marketing.
ReplyDelete