Skip to main content

WAKAZI KIJIJI CHA CHIKOPELO DODOMA WASUBIRI MILIONI 50 ZA KILA KIJIJI


Image result for MAMILIONI YA PESA



Serikali kuchelewa kutoa milioni 50 katika vikundi ndani ya kila kijiji na mtaa kumechangia baadhi ya vikundi ambavyo tayari vilikuwa vimeundwa kusambaratika.

Wakizungumza na Dodoma fm baadhi ya vijana wa kijiji cha chikopelo wilaya ya Bahi katika mkoa wa dodoma wamesema kuwa yapata zaidi ya miaka miwili ahadi ya serikali ya awamu ya tano bado haijatimia ya kuwagawia hizo million 50 jambo linalochangia baadhi ya vikundi vilivyokuwa vimeundwa kuanza kusambaratika kwa kukosa uhakika wa hiyo fedha.

Vijana hao wamesema kuwa awali   baada ya kuunda vikundi hivyo walianza kuchangishana pesa na kukutana mara kwa mara kwa ajili ya kuimarika huku wakisubiri hiyo fedha kutoka serikalini lakini baadaye washirika walianza kutohudhuria na mwisho kusambaratika baada ya kusubiri kwa muda mrefu.

Aidha akitolea ufafanuzi juu wa uwepo wa vikundi vilivyokwisha sambatratika katika kijiji hicho mwenyekiti wa kijiji cha chikopelo Bwana CORNELIUS MAHINYILA amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa vikundi bado viko imara huku vikiendelea kusubiri kutimia kwa ahadi hiyo ya kupokea milioni 50.

Mnamo mwaka 2015 serikali iliyoko madarakani ikiomba lidhaa kwa wananchi ya kuongoza nchi kupitia ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) ilitamka kuwa itatoa shilingi milioni 50 kwa vikundi katika kila kijiji na mtaa fedha ambayo itasaidia mwananchi kujikwamua kiuchumi na kumletea maendeleo.

Hata hivyo serikali kupitia kwa waziri wa fedha na mipango, Dk PHILIP MPANGO imesema ahadi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kutoa Shilingi milioni 50 kila kijiji na mtaa itaanza kutekelezwa mara baada ya mfumo wa kuanza kuzitoa utakapokamilika na kuwakumbusha wananchi kuwa hiyo ni ahadi ya chama kwa kipindi cha miaka mitano.

Na RWEIKIZA  KATEBALIRWE                                 DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

YANGA KESHO KUJUA ANACHEZA NA NANI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

MAJINA ya vigogo wa soka Afrika, wakiwemo mabingwa wa Afrika 1998, Raja Casablanca yametawala katika orodha ya wapinzani wapya wa Yanga kwenye michuano ya Afrika. Yanga SC imeangukia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambako watamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo. Hiyo ni baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Township Rollers Jumamosi jioni Uwanja wa Taifa mjini Gaborone nchini Botswana. Matokeo hayo yanamaanisha Rollers inakwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza historia hiyo kwa ushindi wa jumla wa 2-1 uliotokana na matokeo ya mchezo wa                              kwanza Dar es Salaam Machi 6. Na Yanga SC itamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo, ambazo ni CR Belouizdad, USM Alger za Algeria, Al-Masry ya Misri, Djoliba ya Mali, Raja Casablanca, Enyimba ya Nigeria, SuperSport United ya Afrika K

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifugua kwa upasuaji na