Serikali kuchelewa
kutoa milioni 50 katika vikundi ndani ya kila kijiji na mtaa kumechangia baadhi
ya vikundi ambavyo tayari vilikuwa vimeundwa kusambaratika.
Wakizungumza na
Dodoma fm baadhi ya vijana wa kijiji cha chikopelo wilaya ya Bahi katika mkoa
wa dodoma wamesema kuwa yapata zaidi ya miaka miwili ahadi ya serikali ya awamu
ya tano bado haijatimia ya kuwagawia hizo million 50 jambo linalochangia baadhi
ya vikundi vilivyokuwa vimeundwa kuanza kusambaratika kwa kukosa uhakika wa
hiyo fedha.
Vijana hao wamesema
kuwa awali baada ya kuunda vikundi
hivyo walianza kuchangishana pesa na kukutana mara kwa mara kwa ajili ya kuimarika
huku wakisubiri hiyo fedha kutoka serikalini lakini baadaye washirika walianza
kutohudhuria na mwisho kusambaratika baada ya kusubiri kwa muda mrefu.
Aidha akitolea
ufafanuzi juu wa uwepo wa vikundi vilivyokwisha sambatratika katika kijiji
hicho mwenyekiti wa kijiji cha chikopelo Bwana CORNELIUS MAHINYILA amekanusha
taarifa hizo na kusema kuwa vikundi bado viko imara huku vikiendelea kusubiri
kutimia kwa ahadi hiyo ya kupokea milioni 50.
Mnamo mwaka 2015
serikali iliyoko madarakani ikiomba lidhaa kwa wananchi ya kuongoza nchi
kupitia ilani ya chama cha mapinduzi (CCM) ilitamka kuwa itatoa shilingi
milioni 50 kwa vikundi katika kila kijiji na mtaa fedha ambayo itasaidia
mwananchi kujikwamua kiuchumi na kumletea maendeleo.
Hata hivyo serikali kupitia kwa waziri wa fedha na mipango,
Dk PHILIP MPANGO imesema ahadi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kutoa Shilingi
milioni 50 kila kijiji na mtaa itaanza kutekelezwa mara baada ya mfumo wa
kuanza kuzitoa utakapokamilika na kuwakumbusha wananchi kuwa hiyo ni ahadi ya
chama kwa kipindi cha miaka mitano.
Na RWEIKIZA
KATEBALIRWE DODOMA FM
Comments
Post a Comment