Skip to main content

WADAU WA NISHATI MBADALA WAOMBWA KUTOA ELIMU VIJIJINI


Image result for maadhimisho ya siku ya mazingira dodoma





Naibu mstahiki meya wa jiji la Dodoma amewataka wadau wa nishati mbadala kutembelea vijijni ili kuwafikia wananchi kutoa elimu juu ya matumizi ya nyenzo nyingine za kupata nishati mbadala.

Bwana JUMANNE NGEDE amesema hayo wakati akikagua mabanda ya wadau wa kutoa elimu juu ya utumiaji nishati mbadala katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya mazingira yaliyofanyika Kimkoa katika viwanja vya mwalimu nyerere jijini Dodoma .

Amesema ni vema kila mtu akawa mlinzi wa mwenzake kwa kuhakikisha Dodoma inakuwa safi ikiwemo kutotupa taka hovyo na kuwa atakayekiuka na kukamatwa atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo faini au kifungo.

Akisoma Risala mbele ya mgeni rasmi afisa mazingira wa jiji la Dodoma bwana ALLY MFINANGA amesema uharibifu wa mazingira umesababisha kuzorota kwa shughuri za kiuchumi na kurudisha nyuma maendeleo ya jiji hilo.

Aidha akizungumza kwa niaba ya wadau wa nishati mbadala katika maadhimisho hayo Afisa utawala wa ACO-ACT PROJECT Bi BENEDICTA KIMBE amehaidi kufanyia kazi yote waliyojifunza na kuagizwa ili kuhakikisha wanatokomeza swala la uharibifu wa mazingira.

Maadhimisho ya wiki ya mazingira duniani hufanyika kila ifikapo june 5 kila mwaka na mwaka huu Kitaifa yamefanyika jiji Dar-es-salaam huku yakiwa yamebeba kaulimbiu isemayo mkaa ni gharama tumia njia mbadala na Tupambane kutokomeza taka zitokanazo na plastiki ikiwa ni kauli mbiu ya kimataifa.

NaRWEIKIZAKATEBALIRWE                           DODOMA F

Comments

  1. The Best Slot Machines - The JTM Hub
    The 서산 출장샵 Best Slot 부천 출장마사지 Machines - The JTM 화성 출장마사지 Hub The Best Slot Machines If 울산광역 출장안마 you 경기도 출장안마 want to learn more about this game in our online slot machine guides.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifugua kwa upasuaji na

SERIKALI IMEANZA KUANDAA KITINI CHA MASUALA YA JINSIA

                                             Serikali imeanza mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza katika kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto umekithiri sana nchini   hivyo Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo. Amesema   lengo la kuandaa kitini cha kufundishia masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii. Bi. Mboni amefafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Is