Skip to main content

WADAU WA MAZINGIRA WASHAURIWA KUTUMIA TAKWIMU KUDHIBITI UHARIBIFU


                             Image result for ofisi ya Taifa ya TAKWIMU







Wadau wanaoshughulika na udhibiti wa uharibifu wa mazingira nchini wametakiwa kutumia Takwimu zinazozotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu  kuishauri Serikali kupambana na matumizi ya mkaa kutokana na kuonekana kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa mazingira.

Akiongea na Dodoma Fm Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya TAKWIMU Bw. GODBLESS WILLIAM amesema utafiti uliofanyika mwaka 2016 unaonesha asilimila kubwa ya Watanzania wanatumia  mkaa ambapo mkoa wa Dar es salaam unaongoza kwa asilimia 88 huku Dodoma ikiwa na asilimia 21.

Bw. GODBLESS amesema kwa upande wa matumizi ya kuni Takwimu zinaonesha Lindi ikiongoza kwa asilimia 90 ikifuatiwa na Dodoma yenye asilimia 86. 7 na kwamba misitu imekuwa ikivamiwa kwa asilimia kubwa na wananchi kwa ukataji wa miti kwa ajili ya kuni pamoja na mkaa.

Amesema lengo la Ofisi ya Taifa ya Takwimu ni kuishauri serikali pamoja na wadau wanaopambana na uharibufu wa mazingira kufuatilia takwimu zinazotolewa na kuangalia uwezekano wa kutokomeza uharibifu wa mazingira.

Ili kupata ufafanuzi zaidi juu ya Takwimu za uharibifu wa Mazingira wananchi wa Dodoma wametakiwa kufika katika Ofisi ya Taifa ya Takwimu zilizopo Hazina.


Na Phina Nimrod                                                                DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...