Skip to main content

TAMISEMI YAFUNGUA RASMI MAFUNZO KWA WAHASIBU WA MAMLAKA ZA SERIKALI





Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) wanatoa mafunzo ya kina ya wiki tatu kwa watumishi wa kada  ya uhasibu kutoka  mamlaka  185  za Serikali za Mitaa Tanzania.

 Akifungua mafunzo hayo yanayohusu mfumo  mpya wa Epicor 10.2, leo Jijini Dodoma   Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bibi. Rehema Madenge amesema mafunzo hayo ya mfumo wa Epicor yamelenga kuwapa uelewa Wahasibu juu ya mabadiliko ya maboresho makubwa yaliyofanywa katika mfumo huo.

“Historia inaonesha kuwa Halmashauri zetu zilianza matumizi ya mfumo katika toleo lililojulikana kama Platnum mwaka 1999/2000 na baadaye mfumo ulifanyiwa maboresho na kufungwa epicor toleo Na 7.2 mwaka 2001 wakati huo mfumo ukiwa umefungwa katika Halmashauri 38 tu.” Anasema Bibi
Rehema Madenge.

Aidha ameongeza kwa kufafanua kuwa mwaka 2014/15 mfumo uliboreshwa na kuwa epicor toleo la 7.3.5 na kufungwa katika Halmashauri 44 zaidi hivyo kuwa na Jumla ya Halmashauri 82 zilizokuwa zinatumia mfumo, Rehema Madenge.


Julai Mwaka 2012, TAMISEMI ilifanya maboresho makubwa kwa kuunganisha Halmashauri  133 zilizokuwepo wakati huo kupitia  kampuni ya simu ya taifa TTCL na kuweka epicor toleo namba 9.05 ambalo limeendelea kutumika hadi sasa. Hata hivyo Halmashauri zilizoongezeka baadaye zilifungwa epicor toleo namba 10.1 ambalo limeboreshwa sasa na kuwa 10.2 inayofungwa Halmashauri zote.

Aidha amesema, matumizi ya epicor toleo namba 10.2 ni hatua kubwa sana katika utekelezaji wa dhana nzima ya uwazi uwajibikaji na utawala bora katika usimamizi wa fedha za umma. Hata hivyo amesema, mfumo huo utasaidia Halmashauri kuondokana na vyeti vya hati chafu na zile zenye mashaka kutokana na mapato na matumizi ya fedha zote kutakiwa kuingizwa katika mfumo huo.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mifumo ya Fedha Ofisi ya Rais TAMISEMI Augustino Manda amesema uboreshaji wa mfumo wa Epicor ni muendelezo wa uboreshaji wa mifumo ya Serikali kama ilivyofanyika kwa mifumo mingine kama vile mifumo ya Afya.

Maboresho mengine yaliyofanyika katika mfumo huo wa Epicor 10.2  ni kwamba mifumo yote ya msingi ya usimamizi wa fedha katika sekta za umma kwa sasa itaweza kuwasiliana na kushirikishana taarifa ambapo hapo awali, uongozi na maafisa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa walilazimika kupitia mipango na bajeti katika mfumo mmoja, mapato katika mfumo mwingine na matumizi kwenye mfumo mwingine, hivyo kuleta ugumu katika kudhihirisha uwajibikaji, ufanisi na thamani ya fedha katika matumizi ya fedha za Serikali. 

Vile vile utaunganishwa na mfumo unaowezesha mabenki kulipana Tanzania (TISS) ambao utaruhusu malipo yote kufanyika kwa njia ya kielektroniki. 

Mafunzo hayo yanafanyika katika vituo sita  ambavyo ni Dodoma, Mwanza, Mtwara, Iringa, Kagera na Mbeya yakijumuisha watumiaji wa mfumo huo ambao ni Waweka Hazina na Wahasibu na baadaye Maafisa TEHAMA, Maafisa Manunuzi na Wakaguzi wa Ndani.


Na Zania Miraji                      DODOMA FM 


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...