Skip to main content

SERIKALI YAOMBWA KUZINGATIA VIGEZO VYA USAJILI WAGANGA TIBA ASILI



Image result for WAGANGA TIBA ASILI







Serikali imeombwa kuzingatia vigezo muhimu vinavyotakiwa wakati wa zoezi la kusajili Waganga wa tiba asili ili kuondoa sintofahamu iliyopo kati ya serikali na waganga wa tiba asili ambao wamekuwa wakituhumiwa kujihusisha na imani za kishirikina zinazopelekea uwepo wa mauaji ya watu wenye ualbino nchini.

Kauli hiyo imetoewa na mke wa waziri mkuu mstaafu mama Tunu Pinda wakati akifungua semina ya siku moja mjini Dodoma iliyoandaliwa na shirika la Hope Derivery Foundation iliyowakutanisha watu wenye ualbino na waganga wa tiba asili kwa lengo la kuondoa sintofahamu iliyopo baina ya makundi hayo mawili.

Amesema kuwa serikali ni vyema ikazingatia mambo muhimu wakati wa kuwasajili waganga hao kwa kuwashirikisha viongozi mbalimbali wa maeneo husika  ili kwatambua waganga halali na matapeli na sio kutumia vigezo vya mganga kuwa na matunguli pekee hali itakayosaidia kukomesha mauaji hayo kwanni wengi wao wanaojuhusisha na vitendo hivyo ni wale matapeli.

Kwa upande wake katibu wa waganga wa tiba asili  Joseph Lucas Mlitu amesema kuwa ili kuwabaini waganga wanaojihusisha na vitendo vya mauaji kwa watu wenye ualbino ni vyema serikali ikawashirikisha waganga wenyewe kwani wao ndio wanaowatambua yupi ni mganga wa kweli na yupi ambaye ni tapeli.

Naye mkurugenzi wa shirka la hope derivery  foundation bw, Michael Salali amesema kuwa lengo la kuandaa semina hiyo ni kutoa uelewa kwa waganga wa tiba asili juu ya watu wenye ualbino ili kuondokana na imani potofu kwani tangu mwaka 2006 hadi 2018 tayari zaidi ya watu 79 wenye ualbino wameuawa na wengine kujeruhiwa kwa kukatwa viungo vyao.

NA ALFRED BULAHYA                                             DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...