Waziri wa Nchi
ofisi ya Rais utumishi na utawala bora Kapten George Mkuchika amesema Serikali
ya awamu ya tano inaendelea kuboresha masilahi ya watumishi wa umma na
itapandisha mishahara kwa watumishi hao baada ya hali ya uchumi wa Nchi
kuimarika.
Waziri Mkuchika
ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti
maalumu Mh. Catherin Magige aliehoji Serikali ya awamu ya tano ina mikakati
gani ya kuwajali watumishi wa umma katika masilahi yao.
Kapten Mkuchika
amesema Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali katika kuboresha masilahi
ya watumishi wa umma kwa kuwapatia mikopo, kuwapeleka mafunzo katika taaluma
mbalimbali na zoezi la kupandisha mishahara litafanyika wakati wowote hali ya
uchumi wa Nchi utakapo ruhusu.
Katika hatua
nyingine Kapten Mkuchika amekanusha taarifa za zuio kwa wakurugenzi wa
Halimashauri, Manispaa pamoja na Majiji juu ya kuto kuwatangaza wapinzani iwapo
wameshinda katika chaguzi mbalimbali kutokana na wakurugenzi hao kulipwa
mishahara na Serikali hoja iliyoibuliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mh. Mwita
Waitala
Kapten Mkuchika
amesema swala hilo halina ukweli wowote na badala yake wakurugenzi katika
Halmashauri zote Nchini wamepatiwa mafunzo ya uongozi kwa kuzingatia sheria,
kanuni na taratibu za Nchi ili kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa mjibu wa
sheria.
Na
Pius Jayunga DODOMA FM
Comments
Post a Comment