Skip to main content

SERIKALI YAAHIDI KUPANDISHA MISHAHARA HALI YA UCHUMI ITAKAPOIMARIKA



Image result for Kapten George Mkuchika





Waziri wa Nchi ofisi ya Rais utumishi na utawala bora Kapten George Mkuchika amesema Serikali ya awamu ya tano inaendelea kuboresha masilahi ya watumishi wa umma na itapandisha mishahara kwa watumishi hao baada ya hali ya uchumi wa Nchi kuimarika.

Waziri Mkuchika ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mh. Catherin Magige aliehoji Serikali ya awamu ya tano ina mikakati gani ya kuwajali watumishi wa umma katika masilahi yao.

Kapten Mkuchika amesema Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali katika kuboresha masilahi ya watumishi wa umma kwa kuwapatia mikopo, kuwapeleka mafunzo katika taaluma mbalimbali na zoezi la kupandisha mishahara litafanyika wakati wowote hali ya uchumi wa Nchi utakapo ruhusu.

Katika hatua nyingine Kapten Mkuchika amekanusha taarifa za zuio kwa wakurugenzi wa Halimashauri, Manispaa pamoja na Majiji juu ya kuto kuwatangaza wapinzani iwapo wameshinda katika chaguzi mbalimbali kutokana na wakurugenzi hao kulipwa mishahara na Serikali hoja iliyoibuliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mh. Mwita Waitala

Kapten Mkuchika amesema swala hilo halina ukweli wowote na badala yake wakurugenzi katika Halmashauri zote Nchini wamepatiwa mafunzo ya uongozi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za Nchi ili kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa mjibu wa sheria.

Na Pius Jayunga                                                      DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

YANGA KESHO KUJUA ANACHEZA NA NANI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

MAJINA ya vigogo wa soka Afrika, wakiwemo mabingwa wa Afrika 1998, Raja Casablanca yametawala katika orodha ya wapinzani wapya wa Yanga kwenye michuano ya Afrika. Yanga SC imeangukia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambako watamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo. Hiyo ni baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Township Rollers Jumamosi jioni Uwanja wa Taifa mjini Gaborone nchini Botswana. Matokeo hayo yanamaanisha Rollers inakwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza historia hiyo kwa ushindi wa jumla wa 2-1 uliotokana na matokeo ya mchezo wa                              kwanza Dar es Salaam Machi 6. Na Yanga SC itamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo, ambazo ni CR Belouizdad, USM Alger za Algeria, Al-Masry ya Misri, Djoliba ya Mali, Raja Casablanca, Enyimba ya Nigeria, SuperSport United ya Afrika K

SERIKALI IMEANZA KUANDAA KITINI CHA MASUALA YA JINSIA

                                             Serikali imeanza mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza katika kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto umekithiri sana nchini   hivyo Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo. Amesema   lengo la kuandaa kitini cha kufundishia masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii. Bi. Mboni amefafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Is