Serikali imesema
haina jukumu la kugharamia huduma za mazishi wazazi wa mtumishi wa umma wanapofariki kutokana na
baadhi ya wazazi kuwa na watoto zaidi ya mmoja.
Naibu waziri ofisi
ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEM) Mh. Joseph Kakunda
ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri ofisi ya Rais
utumishi na utawala bora wakati akijibu swali la Mbunge Kosato Chumi aliehoji
ni lini Serikali itawajumuisha wazazi wa mtumishi kama wanufaika wa huduma
mbalimbali anazopata mtumishi wa umma.
Amesema kwa mujibu
wa kanuni za kudumu katika utumishi wa umma inaelekeza huduma za mazishi
kutolewa kwa mtumishi mwenyewe pamoja na wategemezi wa nne na uwepo wa kanuni
hiyo imesaidia Serikali kuepuka kulipa gharama zaidi ya mara moja kwa mzazi
mmoja aliefariki kutokana na kuto kuwepo kwa mfumo wa kutambua wazazi wenye
watoto zaidi ya mmoja katika utumishi wa umma.
Mh. Kakunda amesema
ili kuziba pengo lililopo katika kuhudumia mazishi ya wazazi Serikali imeruhusu watumishi wa umma
kuchangiana kupitia vyama vya hiari michango ambayo hufunguliwa akaunti maalumu
ili kupeana rambirambi wakati mtumishi anapofiwa na mzazi wake mfumo ambao
ulianzishwa na umoja wa watumishi.
Katika hatua
nyingine Mh. Kakunda ametoa rai kwa watumishi wa umma kujenga tabia ya
mahusiano mazuri mahali pa kazi hatua inayoweza kurahisisha watumishi hao
kusaidiana wao kwa wao badala ya kutegemea kuingizwaa katika mfumo rasmi wa
kugharamiwa na Serikali hasa pale mtumishi anapofiwa na mzazi.
Na
Pius Jayunga
DODOMA FM
Comments
Post a Comment