Skip to main content

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WAGANGA WA TIBA ASILI KUBAINI WANAOUA ALBINO


                                   Image result for ALBINO      







Serikali imeahidi kutoa ushirikiano kwa waganga wa tiba asili katika jitihada za kuwabaini watu wanaojihusisha na mauaji ya vikongwe na watu wenye Ualbino.

Hatua hiyo imekuja kufatia hivi karibuni waganga wa tiba asili kuomba kupewa ushirikiano na serikali wakati wa zoezi la kusajili waganga hao ili kubaini waganga wabaya na wazuri jambo ambalo litasaidia kuwabaini waganga matapeli wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Akiongea na umoja wa waganga wa tiba asili na wakunga (UWAWATA) pamoja na watu wenye ualbino Mwenyekiti wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mussa Zungu amesema kuwa waganga wabaya wataendelea kuwepo iwapo wateja wabaya watakuwepo hivyo waganga wote watoe ushirikiano kwa vyombo vya dola ili hatua zichukuliwe dhidi ya wale watakaobainika.

Naye kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto amewataka kuanza kuibainisha mikoa iliyo na matukio mengi ya aina hiyo pamoja na kutoa elimu katika mikoa mbalimbali hapa inchini ikiwemo mkoa wa kagera kwani ndio unaotajwa kuwa na vitendo vingi vya mauaji.

Hata hivyo ili kuendelea kuboresha mahusiano baina ya waganga wa tiba asili na watu wenye ualbino nchini mwenyekiti wa waganga hao Bwana Bujukano Mahungu John kwa niaba ya umoja wa waganga hao akamtangaza mkurugenzi wa Taasisi ya Hope Derivery Foundation inayoshughulika na masula ya kupinga ukatili kwa watu wenye ualbino Bwana  Michael Salali kuwa mratibu wa umoja huo hapa nchini.

NA ALFRED BULAHYA                                                      DODOMA FM

Comments

  1. We are providing online services to customer for SEO and search engine marketing (SEM). They produce more effect result within one month. I am advising you please do not wash your money and time. they are generating organic results and different types of full package on monthly basis.Thank You

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

YANGA KESHO KUJUA ANACHEZA NA NANI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

MAJINA ya vigogo wa soka Afrika, wakiwemo mabingwa wa Afrika 1998, Raja Casablanca yametawala katika orodha ya wapinzani wapya wa Yanga kwenye michuano ya Afrika. Yanga SC imeangukia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambako watamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo. Hiyo ni baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Township Rollers Jumamosi jioni Uwanja wa Taifa mjini Gaborone nchini Botswana. Matokeo hayo yanamaanisha Rollers inakwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza historia hiyo kwa ushindi wa jumla wa 2-1 uliotokana na matokeo ya mchezo wa                              kwanza Dar es Salaam Machi 6. Na Yanga SC itamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo, ambazo ni CR Belouizdad, USM Alger za Algeria, Al-Masry ya Misri, Djoliba ya Mali, Raja Casablanca, Enyimba ya Nigeria, SuperSport United ya Afrika K

SERIKALI IMEANZA KUANDAA KITINI CHA MASUALA YA JINSIA

                                             Serikali imeanza mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza katika kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto umekithiri sana nchini   hivyo Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo. Amesema   lengo la kuandaa kitini cha kufundishia masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii. Bi. Mboni amefafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Is