Skip to main content

RAIS MAGUFULI AZINDUA MPANGO WA MAENDELEO YA KILIMO AWAMU YA PILI







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amesema njia pekee itakayosaidia kuinua sekta ya kilimo Nchini ni ma afisa ugani kutumia matokeo ya utafiti pamoja na kuimarisha vituo vya utafiti vya kilimo Nchini ili kuongeza fursa ya uzalishaji.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jijini Dar es salaam wakati akizindua mpango wa maendeleo ya kilimo awamu ya pili ambapo amesema iwapo maafisa ugani watatumia matokeo ya utafiti katika sekta ya kilimo yatasaidia kuinua sekta ya kilimo hapa Nchini.

Amesema chuo kikuu cha sokoine kina wajibu mkubwa wa kusaidia sekta ya kilimo kwa kufanya tafiti nyingi ikiwemo kubuni teknolojia mpya ambayo ni rahisi kwa wakulima kama kuhifadhi mazao, kubuni dawa na mbinu za kupambana na magonjwa ya mimea pamoja na kuanzisha mashamba darasa katika maeneo mbalimbali Nchini.

Aidha Rais Magufuli ameeleza kuto kuridhishwa na utendaji kazi wa Bank ya maendeleo ya kilimo Nchini (TADB) na kubainisha kuwa kwa sasa Nchi ina jumla ya hekta milioni 44, na hekta milioni 29.4 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji na katika mifugo Tanzania ikishika nafasi ya pili kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo barani afrika ikifuatiwa na Ethiopia.

Nae waziri wa kilimo, mifugo na uvuvi Dr. Charles Tizeba amesema sekta ya kilimo ina uhusiano wa moja kwa moja na sekta ya viwanda kutokana na baadhi ya malighafi ambazo huzalishwa katika kilimo hutumika pia katika kuzalisha bidhaa viwandani na kwamba kwa mwaka 2016/17 jumla ya viwanda vitumiavyo malighafi kutoka sekta ya kilimo vimeongezeka kutoka viwanda 49243 hadi viwanda 52546 mwaka mwaka 2016/17.

Na Pius Jauynga                                                             DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...