Skip to main content

'MKAA NI GHARAMA TUMIA NISHATI MBADALA'



Image result for MKAA




Kuelekea maadhimisho ya siku ya mazingira duniani jamii mkoani Dodoma imetakiwa kuhakikisha inatumia vyombo maalumu vilivyoko katika maeneo yao kuweka uchafu ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuimarisha usafi nchini.

Wito huo umetolewa leo na kaimu afisa mazingira wa jiji la Dodoma bw, Ally Mfinanga, wakati akiongea na DODOMA FM ikiwa ni siku moja tu imesalia ili kufikia kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira duniani.

Amesema kuwa jamii inapaswa kuvitumia vyombo hivyo kwani vimewekwa kwa ajili ya kazi hiyo ili kuepusha suala la utupaji wa taka hovyo hivyo kila mmoja Anatakiwa kuzingatia jambo hilo ili kuliweka jiji la Dodoma katika hali safi.

Akizungumzia hali ya usafi katika jiji la Dodoma amesema kuwa hali inaendelea kuimarika licha ya elimu ya usafi kuwa ndogo katika jamii huku akisisitiza wananchi kufanya mabadiliko ya kuhakikisha usafi unaimarika katika meneo yao ili kuepusha usumbufu wa kuchuliwa hatua ikiwemo kutozwa faini.

Baadhi ya wananchi wa jiji la Dodoma wameimbaia Taswira ya habari kuwa kwa sasa hali ya usafi inaendelea kuimarika mkoani hapa na kwamba serikali inapaswa kuendelea na jitihada za kuhamamsisha suala la usafi kwani wapo baadhi ya wananchi bado hawana elimu sahihi juu ya utunzaji wa mazingira.

Maadhimisho ya siku ya mazingira duniani huadhimishwa kila mwaka  ifikapo june 5 na kwa mwaka huu mkoa wa Dodoma yatafanyika katika viwanja vya Nyerere  Square huku kitaifa kilele cha maadhimisho hayo kitafanyika Jijini Dar es salaam kikiwa na kauli mbiu isemayo mkaa ni gharama tumia nishati mbadala, na kimataifa kauli mbiu inasema Tuongeze nguvu katika kupambana na taka zitokanazo na plastiki.

NA ALFRED BULAHYA                                 DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...