Skip to main content

MIPANGO YA SERIKALI JUU YA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA


Image result for WAZIRI MAVUNDE






Katika kuhakikisha tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana nchini linatatuliwa Serikali imesema inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ili kukabiliana na tatizo.

Naibu Waziri ofisi ya Waziri mkuu sera, bunge, kazi, ajira na watu wenye ulemavu Mh. Athony Mavunde ameyasema hayo leo Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mh. Asha Abdul Juma alietaka kujua ni lini Serikali itafanya juhudi za dhati kulishughulikia swala hilo ili kuongeza fursa ya ajira.

Naibu waziri Mavunde amesema Serikali imetoa kipaumbele kwa vijana waliohitimu elimu ya vyuo vya ufundi kwa kupewa kipaumbele hasa katika mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa, ujenzi wa bomba la mafuta, mradi wa usambazaji umeme vijijini pamoja na mradi wa kufua umeme na katika mradi wa bomba la mafuta zaidi ya nafasi elfu 11 za ajira mbalimbali zitapatikana.

Aidha Mh. Mavunde amesema Serikali imeainisha aina ya ujuzi unaohitajika katika  ujenzi wa miradi husika na tayari imetenga fedha za kugharamia pengo la ujuzi lililopo kati ya wahitimu pamoja na soko la ajira na kwamba kupitia mfuko wa maendeleo ya vijana Serikali imeendelea kutoa mikopo yenye mashariti nafuu.

Amevitaja  vituo vya vijana vilivyopo chini ya  ofisi ya Waziri mkuu kuwa ni pamoja na kituo cha vijana Sasanda Mbozi, kituo cha vijana Ironga kilosa pamoja na kilimanjaro vituo ambavyo vipo kwa ajili ya kuwalea vijana pamoja na kuwaandaa kuwa na sifa za kuajirika.

Na Pius Jayunga                                                         Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...