Skip to main content

MAPACHA MARIA NA CONSOLATA WALIOFARIKI DUNIA JUMAMOSI WAAGWA LEO IRINGA


                              Image result for consolata na maria



Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amewataka Watanzania hususani wazazi na walezi kuto kuwaficha watoto walio na ulemavu kwa kuwapatia haki ya kupata elimu.

Prof. Ndalichako ameyasema hayo leo wakati akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kuaga miili ya Marehemu Maria pamoja na Consolata waliofariki Dunia mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Iringa.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imetoa kipaumbele kwa kundi la watu wenye ulemavu kwa kuwapatia elimu na kwamba jamii inapaswa kuunga mkono juhudi hizo kwa kuwapeleka shule watoto walio na ulemavu ili kupatiwa haki hiyo stahiki.

Naibu Waziri ofisi ya Waziri mkuu anaeshughulikia maswala ya watu wenye ulemavu Mh. Stella Ikupa amesema baadhi ya watu wenye ulemavu wamekuwa wakishindwa kujiamini kutokana na malezi yatolewayo katika familia zao kwa kukatishwa tamaa jambo ambalo jamii inapswa kulipinga na kuwatetea watu walio na ulemavu.

Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, mkuu wa Wilaya ya Makete Bi. Veronica Kesi amesema Maria na Consolata wameacha somo kwa jamii juu ya umuhimu wa kuwapatia nafasi watu walio na ulemavu ili kuonesha uwezo wao hasa katika upande wa elimu.

Mapacha walioungana Maria na Consolata walifariki Dunia siku ya jumamosi june 2, 2018 wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Iringa na enzi za uhai wao mapacha hao walifanikiwa kuanza masomo ya juu katika chuo kikuu cha katoliki cha Ruaha cha mjini Iringa  baada ya kufaulu katika mitihani yao ya kidato cha sita.

Na Pius Jayunga                                                     DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...