Katika kuelekea
sikukuu ya Eid alfitiri Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limeendelea kuimarisha
ulinzi ili kuhakikisha sikukuu inasheherekewa kwa utulivu pamoja na kuwakamata wahalifu wa makosa
mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma GILLES
MUROTO amesema jeshi la polisi limekuwa likifanya msako wa nyumba kwa nyumba
ili kuhakisha wanadhibiti uhalifu na wahalifu na wote watakaokamatwa
watafikishwa mahakamani.
Kamanda MUROTO amesema jeshi la polisi limekamata zaidi ya watu 25 kwa
makosa tofauti tofauti ikiwemo ya uvunjaji, utapeli, bangi na uuzaji wa bidhaa
za vipodozi vyenye viambata vya sumu.
Sambamba na hayo ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za
wahalifu na uhalifu ili jiji la Dodoma liweze kuwa shwari wakati wote.
Kwa upande wao wananchi wamesema ni vyema vijana wa kafanya kazi kwa
bidii na kuliomba jeshi la Polisi liendelee kuchukua hatua kwa wahalifu
wanaowakamata.
Na Phina Nimrod
DODOMA FM
Comments
Post a Comment