Uongozi wa jiji la Dodoma umewaomba wananchi kuendelea kudumisha hali ya usafi ili jiji la
Dodoma liweze kuibuka kidedea katika mashindano ya kitaifa ya usafi wa mazingira.
Ushindanishwaji
huo utayahusisha majiji yote nchini, jiji la Dodoma likiingia kwa mara ya
kwanza katika kinyang’anyiro hicho, na uongozi wa Jiji hilo kuahidi ushindi.
Akielezea
namna jiji la Dodoma lilivyojipaga
kufanya vizuri katika utunzaji wa mazingra na kupata ushindi, mkuu wa
idara ya mazingira na udhibiti wa taka ngumu jiji Dodoma bwna Dickson Kimaro
amesema mkoa haupo tayari kumuangusha rais kwa maamuzi yake yenye busara ya
kuufanya Mkoa wa Dodoma kuwa jiji, na kuwataka wananchi wote kushiriki
kuyatunza mazingira.
Aidha
bwna Kimaro amewataka watu kuacha kutupa taka kiholela, badala yake watupe
katika maeneo yaliyoanishwa, na kwamba mtu yeyote atakaye kwenda kinyume na
maelekezo atawajibishwa kwa mujibu wa sheria.
Kwa
upande wake afisa afya mkoa wa Dodoma bwna Kale Limo amewataka watu wanaoinga
ndani ya jiji la Dodoma wakitokea maeno ya nje ya jiji, wazingatie usafi
hususani kutupa taka maeneo yaliyoelekezwa na Uongozi wa jiji.
Ikumbukwe
kuwa ushindanishwaji huu utafanyika kuanzia tarehe 13 juny 2018, huku Dodoma
ikiwa na mwezi mmoja tangu itangazwe kuwa jiji
Na Victor Makwawa
DODOMA FM
Comments
Post a Comment