Skip to main content

ELIMU YA UCHANGIAJI DAMU BADO INAHITAJIKA







                               Image result for KITENGO CHA DAMU SALAMA DODOMA



Katika kuelekea Maadhimisho ya siku ya uchangiaji damu Duniani ambayo huadhimishwa  kila mwaka June 14  jamii imeomba kupewa elimu ili waweze kuondokana na imani potofu walizonazo juu ya uchangiaji damu.

Wakizungumza na Dodoma fm baadhi ya wananchi wamesema kitengo cha damu salama kimekuwa hakitoi elimu kwa wananchi na badala yake kimelenga kutoa elimu mashuleni kitendo ambacho hupelekea wachangiaji damu wengi kuwa wanafunzi.

Kutokana na wananchi kutokupata elimu ya uchangiaji damu hii imepelekea kuwepo kwa mtazamo hafifu juu ya swala la kuchangia damu ambapo wengi wao wamekuwa wakidhani uchangiaji wa damu unaweza kumpelekea mwanachama kuishiwa damu.

Akizungumzia juu ya vigezo vya uchangiaji damu msimamizi mkuu wa kitengo cha damu salama Jijini Dodoma Dokta Leah Kitundya amesema ili mtu aweze kuchangia damu ni lazima awe na uzito usipungua Kilo  50 na asiyekuwa na magonjwa nyemelezi.

Aidha amesema mbali na damu kuokoa maisha mchangiaji anaweza kufahamu afya yake kuwa salama kwa kigezo cha kuchangia damu,kupata cheti cha uanachama  pamoja na kujifahamu kuwa yupo kundi gani la damu .

Maadhimisho ya uchangiaji damu  kwa  mwaka huu yatafanyika uwanja wa Mwalimu nyerere jijini Dodoma yakiwa na lengo la  kutoa zawadi kwa washiriki ambao wamekuwa wakichangia damu pamoja na kutoa elimu kwa jamii juu ya uchangiaji wa damu.

Na ANIPHA RAMADHANI                                              DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...