Skip to main content

ZAIDI YA BILIONI MIA TATU ZALIPWA MALIMBIKIZO YA MAFAO YA WASTAAFU


Image result for WAZIRI MHAGAMA







SERIKALI imesema hadi kufikia mwaka 2017/18 tayari imekwisha lipa deni la Shilingi billion 309.77 kati ya deni la shilingi bilion 413.96 la malimbikizo ya mafao ya wastaafu wanaolipwa kupitia Bank kuu.

Malipo hayo ni sawa na asilimia 74.83 ya malipo ya deni hilo huku ikitabainisha kuwa hadi sasa imekwisha lipa jumla ya Shilingi Tirion 1.36 ikiwa ni  deni lote la malimbikizo ya michango ya wastaafu kupitia mifuko ya hifadhi za jamii.

Hayo yameelezwa na Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Wazee,Vijana na Watu wenye ulemavu Mh.Jenista Mhagama Jijini Dodoma wakati akizindua mpango wa mikopo ya wastaafu iliyoandaliwa na Bank ya NBC.

Mbali na kuipongeza Bank hiyo kwa mpango huo Mhagama amesema kama Serikali sasa imeamua kulipa madeni ya wastaafu ili kuwapa mwanya wa kutumia mafao yao kupata mikopo.

Waziri Mhagama ameongeza kuwa mara baada ya kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii Serikali itahakikisha inatengeneza mfumo utakaowezeha wastaafu wote wanapata mafao yao pasi kuwepo kwa usumbufu na vikwazo vya kuchelewa kwa mafao yao.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Bank ya NBC Tanzania Theobald Sabi ametaja sababu zilizowapelekea kuanzisha mikopo hiyo kwa wastaafu kuwa ni pamoja na kuwasaidia kuendesha maisha yao mara baada ya kustaafu.

Nao baadhi ya wastaafu waliohudhuria katika uzinduzi huo wameipongeza Bank ya NBC na kusema sasa wamepata nguvu mpya ya kuendeleza maisha yao.

Na MARIAM MATUNDU                            CHANZO:DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...