Skip to main content

WIZARA YA AFYA YASEMA HAKUNA TATIZO LA DAWA WALA VIFA TIBA NCHINI.


Image result for NAIBU WAZIRI WA afya ndugulile






Serikali kupitia Wizara ya Afya imesema haina changamoto ya upatikanaji wa dawa  wala fedha kwa ajili ya vifaa tiba pamoja na vitendea kazi.

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mh. FAUSTINE NDUNGULILE amebainisha hayo na kueleza kuwa  changamoto iliyopo ni kwa watoa huduma kuwa na mawazo ya kipindi cha nyuma ya ukosefu wa vifaa.

Naibu waziri huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya uwepo wa changamoto ya upatikanaji wa dawa pamoja na vifaa tiba nchini.

Mh Ndungulele amesema kuwa mara nyingi wizara imekuwa ikipata taarifa ya kuwepo kwa changamoto ya ukosefu wa baadhi ya vitu hivyo lakini wanapofuatilia hugundulika kuwa baadhi ya watoa huduma hawafuatilii vitu hivyo  MSD.

Katika hatua nyingine Ndungulele amesema kumekuwa na ongezeko la watu katika Mkoa wa Dodoma  kutokana na serikali kuhamia   hivyo serikali inatambua kuwepo kwa changamoto ya Chumba cha kuhifadhi maiti  hivyo katika bajeti inayokuja Wizara hiyo imeweka kipaumbele katika suala hilo.

Akizungumzia gharama za matibabu Ndungulile amesema serikali imedhamiria kuja na mfumo wa bima ya afya kwa mwananchi mmoja mmoja ili kila mwananchi aweze kufaidika na bima ya afya.

Na Phina Nimrod                                                         Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...