Skip to main content

WAZIRI MWIGULU AWAONYA MADEREVA BODABODA WASIOTII SHERIA

Image result for waziri MWIGULU






Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na Jeshi la Polisi Nchini imebainika kuwa ajali za barabarani zinasababishwa na vyanzo vikuu vitatu ikiwemo  vya kibinadamu 76%, vya kiufundi 16% na vya  kimazingira  kwa asilimia 8.

Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Dr. Mwigulu Nchemba ameyabainisha hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tabora Mjini Mh. Emmanuel Adam Sony alietaka kujua Serikali ina mkakati gani kuhakikisha ajali za kizembe zinazosababishwa na baadhi ya askari Polisi zinakomeshwa.

Dr. Mwigulu amesema katika vyanzo vya kibinadamu kuna uzembe ambao umekuwa ukijitokeza hasa kwa waendesha pikipiki ambao wamekuwa na uelewa mdogo juu ya sheria za usalama barabarani na kutokana na sababu hizo waendesha pikipiki hujihisi wana makosa wakati wowote wanapoendesha vyombo vyao wakihofia kukamatwa na Polisi.

Amesema ni wajibu wa askari Polisi kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa na waendesha pikipiki wanapaswa kutambua hilo na kutimiza wajibu wao wa kufuata sheria badala ya kumkwepa askari kutokana na makosa yanayojitokeza .

Akielezea juu ya kima cha faini anayopaswa kutozwa dereva bodaboda Waziri Mwigulu amesema swala hilo linatarajiwa kupitishwa kupitia bajeti ya Wizara ya fedha na mipango ili kutofautisha faini wanayotozwa madereva bodaboda, mabasi pamoja na vyombo vingine vya usafiri.

Na Pius Jayunga                                                  Dodoma FM                                                                                      

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...