Skip to main content

WAZIRI MKUU ASEMA SERIKALI IKO MBIONI KUTOA HUDUMA YA CHAKULA KWA WANAFUNZI WA KUTWA

                Image result for waziri mkuu kasimu majaliwa





Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasimu Majaliwa amesema Serikali ipo katika mkakati wa kupanga bajeti ya utoaji wa huduma ya chakula kwa wanafunzi katika shule za sekondari za kutwa zikiwemo pia shule za msingi kote Nchini.

Waziri mkuu Kasimu Majaliwa ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma katika kikao cha 26 mkutano wa 11 katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Temeke Abdalha Mtolea aliehoji ni lini Serikali itabadilisha sera ya elimu ili utoaji wa huduma ya chakula kwa wanafunzi itambulike rasmi.

Waziri Mkuu amesema Tanzania ina jumla ya shule milioni 17 idadi ya shule za sekondari zikiwa 3547 na kwamba serikali imeanza kutoa huduma hiyo kwa wanafunzi wa shule za sekondari za kutwa huku zoezi hilo likiendelea kuratibiwa ili kuwafikishia huduma hiyo wanafunzi wa shule za msingi kote nchini.

Mh. Kasimu Majaliwa amesema baada ya Serikali kuanza kutoa elimu bure imesaidia watoto wengi kupata elimu na kueleza kuwa ni jukumu la wazazi na walezi kushirikiana na Serikali hasa katika kufanikisha upatikanaji wa huduma ya chakula kwa wanafunzi.

Baada ya kukamilika kwa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri mkuu wabunge wameendelea na maswali ya kawaida ambapo Mbunge wa viti maalumu Zainabu Mdolo Amiri amehoji ni lini Serikali itapunguza gharama ya gesi kwa matumizi ya nyumbani ili kuwawezesha wanachi wengi kupata huduma hiyo na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa nishati Mh. Subira Mgaru amesema mikakati ya kuunganisha gesi majukumbani inaendelea na katika awamu ya kwanza mradi huo utapita katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam na Mtwara kisha kusambaza huduma hiyo katika maeneo yote Nchini.

Na Piud Jayunga                                                  Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...