Skip to main content

WAZEE JIJINI DODOMA WANEEMEKA NA MPANGO WA VITAMBULISHO VYA KUPATA MATIBABU BURE



Image result for WAZEE KUPATIWA VIBALI VYA KUPATA MATIBABU






Jumla ya wazee 15,854 walio na zaidi ya miaka 60 kutoka kata mbalimbali za mkoa wa Dodoma wanatarajia kupewa vitambulisho maalumu vitakavyowasaidia kupata matibabu bure katika hospitali mbalimbali zilizopo hapa nchini.

Hayo yamebainishwa leo na Mganga mkuu mkoa wa Dodoma Dkt Hamad Nyembea wakati akizungumza na kituo hiki ambapo amesema kuwa wazee kutoka katika kata 33 wametambulika ili kupatiwa vitambulisho kwa ajili ya kupatiwa matibabu bure.

Amesema kuwa lengo la kutoa vitambulisho hivyo ni kuhakikisha wazee wanatambulika na kupewa fursa kwenye shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwa ni pamoja na kupatiwa matibabu na kwamba wazee 1,118  tayari wamekwishapigwa picha kwa ajili ya zoezi hilo huku wengine 355 kutoka kata ya Mkonze mkoani hapa tayari wamepatiwa vitambulisho hivyo.

Aidha ameongeza kuwa awali wazee katika maeneo mbalimbali walikuwa wakipata taabu pindi wanapohitaji matibabu na kupitia vitambulisho hvyo vitawasaidia katika nyanja mbalimbali katika maisha yao na kwamba kuanzia wiki ijayo zoezi hilo litaendelea katika maeneo mengine mkoani hapa.

Kwa upande wao baadhi ya wazee waliopatiwa vitambulisho hivyo wameishukuru serikali kwa hatua hiyo huku wakiitaka serikali kuhakikisha inatoa huduma za uhakika kwani ipo changamoto ya kokosa huduma kikamilifu kwa wazee hao kama kutakiwa kununua dawa katika maeneo mengine ya nje ya hospitali wanazokwenda  licha ya kupewa vitambulisho hivyo.

Ikumbukwe kuwa wiki iliyopita waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Seleman Jafo akiwa katika zoezi la utoaji wa vitambulisho hivyo kwa wazee wa kata ya Mkonze alitoa muda wa siku 34 kuhakikisha kila mkoa unatoa taarifa za kuwatambua wazee kwani jambo hili limekuwa likipigiwa kelele kwa mda mrefu bila mafanikio na watakaoshindwa kutekeleza serikali haitasita kuwachukulia hatua.

NA ALFRED BULAHYA                                                     DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...