Skip to main content

WAZAZI WATAKIWA KUWAPA NAFASI WATOTO KUJUA MZAZI WA PILI



Katika kudai haki ya msingi ya kumjua mzazi wa upande wa pili baba au mama katika familia walengwa ambao ni watoto wazawa wameshauriwa kubuni mbinu sahihi na kufuata taratibu ili kufanikisha lengo pasipo kupata madhara.

Ushauri huo unakuja baada ya baadhi ya familia kuwa na migogoro inayohusisha watoto na wazazi wao chanzo kikiwa ni pale mtoto anapoanza kudai haki yake ya msingi ya kutaka kumjua mzazi wake wa upande wa pili wa kike au wa kiume jambo ambalo huzua tafrani.

Akizungumza na Dodoma FM ofisini kwake mwanasheria kutoka National Attorney Advocates jijini Dodoma Bwana PAUL KUSEKWA amesema migogoro katika familia inayohusu watoto kudai kumjua mzazi wa upande wa pili bado ni tatizo hivyo amewaomba watoto kutumia njia sahihi za kupata ufumbuzi pasipo kuleta madhara huku akiwaomba nao wazazi husika kuwaonesha watoto wao wazazi wa pili kwani ni haki yao.

Amesema kudai haki kwa kutotumia taratibu kunaweza kuzua mijadala mingine na mikubwa ikiwemo kupoteza haki yako ya msingi kabisa huku akisema swala la kwa nini mzazi hataki kumwonyesha mtoto wake baba au mama inatokana na historia yao tangu kukutana.

Aidha amesema mtoto kukosa haki ya kuwajua  wazazi wa pande  zote mbili kunachangia kukosa mahitaji yake muhimu kama elimu chakula na malazi,huku akisema  asilimia kubwa ya migogoro inayoendelea katika familia ya kumdai mzazi wa pili inaonesha wazazi wa kike wanaongoza kulalamikiwa kwa kutowaonesha watoto wao wazazi wao wa kiume.

Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                                  DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...