Skip to main content

WATANZANIA WAISHIO MPAKANI WATAHADHARISHWA DHIDI YA HOMA YA EBOLA

Image result for waziri Ummy




Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto imetoa tahadhari kwa Wananchi wa Tanzania juu ya Ungonjwa wa Ebola  hasa katika mikoa inayopakana na nchi Jirani ya Jamhuri  ya Kidemokrasia ya Kongo.

Akiongea na Waandishi wa Habari mapema leo mjini Dodoma Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu amesema Tanzania inapakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hivyo ipo hatarini kuambukizwa ugonjwa huo kutokana na mwingiliano wa watu hasa wasafiri wanaotoka na kuingia nchini.

Waziri Ummy ameitaja mikoa inayopakana na Nchi hiyo kuwa ni Mwanza, Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa na Songwe.

Amesema ugojwa wa Ebola husababishwa na virusi vya Ebola ambavyo huambukiza kwa njia ya kugusa damu au majimaji kutoka kwa mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo, kugusa maiti ya mtu aliyekufa kwa ugonjwa huo pamoja na kugusa wanyama walioambukizwa.

Akizitaja dalili za ugonjwa wa Ebola Waziri Ummy amesema huanza kuonekana kwa mtu aliyeambukizwa baada ya siku 2 hadi 21 tangu kupata maambukizi na kwamba  mtu atakuwa na homa kali ya ghafla, kulegea kwa mwili, maumivu ya misuli pamoja na kuumwa kichwa na vidonda kooni.

Sambamba na hayo amesema ili kujikinga na ugonjwa huo ni kuepuka kugusa au kuingiwa na mate, damu, mkojo, kinyesi, machozi na majimaji mengine yanayotoka katika mwili wa mtu mwenye dalili za ugonjwa huo.

Wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu bali kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa huo na kwamba mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitishwa kuugua ugonjwa huo hapa nchini.

Na Phina Nimrod                                                                   Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...