Skip to main content

WATANZANIA SASA KUPIMA UKIMWI KWA KUTUMIA MATE


Image result for WAZIRI WA AFYA







Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amesema Serikali kupitia wizara ya afya imekamilisha maandalizi ya kuwezesha watu kujipima wao wenyewe maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kutumia mate.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo katika mkutano wa 11 kikao cha 41 cha Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Jimbo la Mtambulie Masoud Abdalla Salim aliehoji mkakati wa Serikali kutambua watu wanaoathirika na maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Waziri Ummy amesema mkakati wa Serikali uliolenga kuwapa watu fursa ya kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi  umekamilika na tayari mwanasheria mkuu wa Serikali amekwisha kuandikiwa barua ili kuleta mabadiliko madogo ya sheria itakayoruhusu mtu kujipima maambukizi ya virusi vya ukimwi na kuyapata majibu ndani ya dakika 15.

Nae Waziri ofisi ya Waziri mkuu sera, Bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Mh. Jenista Mhagama amesema baada ya kuzinduliwa kwa takwimu za ukimwi kwa mwaka 2017 imesaidia kujua hali ya ukimwi kutoka Mkoa mmoja hadi mwingine na kwamba tume ya kudhibiti ukimwi Nchini TACAIDS imepewa jukumu la kuhakikisha kila Mkoa unatengeneza mkakati wa kutokomeza maambukizi hayo kulingana na takwimu za mkoa husika.

Kwa upande wake naibu Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr. Faustine Ndugulile amesema takwimu za maambukizi ya virusi vya ukimwi Nchini ziko sahihi na huratibiwa na Serikali kupitia taasisi ya TACAIDS pamoja na wizara ya afya kitengo cha ukimwi ambao ndio waratibu wakuu wa takwimu hizo.

Na Pius Jayunga                                            BUNGE/Dodoma FM  

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...