Skip to main content

WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA IDARA YA UHAMIAJI KUDHIBITI UHAMIAJI HARAMU

                   
Image result for IDARA YA UHAMIAJI




Idara ya uhamiaji mkoani Dodoma imewataka wananchi wote wanaoishi katika jiji la dodoma kufuata sheria ,kanuni  na taratibu za uhamiaji kama inavyotakiwa ili kuendelea kutokomeza wimbi la uwepo wa wahamiaji haramu.

Hatua hiyo imekuja kufuatia mkoa wa Dodoma kupandishwa hadhi ya kuwa jiji na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya muungano wa Tangnyika na Zanzibar ambao huadhimisha kila mwaka ifikapo april 26.

Akizungumza leo na taswira ya habari ofisini kwake afisa uhamiaji mkoa wa Dodoma Bwana Peter Kundi amesema kuwa tayari wamejipanga kuimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ikiwemo nyumba za kulala wageni ,maeneo ya mikusanyiko ya watu na katika barabara zinazoruhusu watu kuingia na kutoka mkoani hapa kwa lengo la kupambana na wahamiaji haramu ambapo wamekuwa wakitajwa kuwa chanzo cha uhalifu hapa nchini.

Katika hatua nyingine amewataka wananchi kuwa wazalendo kwa kuacha kuwahifadhi wahamiaji haramu katika maeneo mbalimbali na badala yake kujenga desturi ya kutoa taarifa kwa vyombo husika pindi wanapobaini uwepo wa wahamiaji haramu ili kuendelea kulinda usalama wa nchi kwani jukumu hilo ni la kila mwananchi.

NA ALFRED BULAHYA                                                   DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...