Skip to main content

WAKAZI WA SWASWA DODOMA HAWAKO TAYARI KUTII AGIZO LA NAIBU WAZIRI KANGI LUGOLA

 Image result for Maji taka kupigwa marufuku Swaswa





Licha ya kutoa elimu kwa wananchi waishio Swaswa  Jijini Dodoma wanaojihusisha na kilimo kwa kutumia maji taka yanayotajwa kuwa na madhara bado ni changamoto kwa wananchi hao.

Akizungumza na Dodoma FM Eng.KASHILIMU MAYUNGA Kutoka  Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Dododma DUWASA  amesema wamefanya jitihada ya kutoa elimu kwa kufanya vikao mabalimbali lakini wananchi hao wanadai kuwa hawako tayari kuondoka katika eneo hilo.

Eng.KASHILIMU amesema licha ya kuweka walinzi katika eneo hilo ambao wanazuia wananchi kuyatumia maji taka hayo bado utekelezaji ni mgumu  kwa  wananchi ambao wanasema hawawezi kuondoka na kuacha kwa madai kuwa yanawasaidia katika kilimo.

Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha mawasiliano kutoka mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira DUWASA Bwana SEBASTIAN WARIOBA  amesema mpaka sasa wamechimba mtaro mrefu wa kudhibiti maji hayo na wamepiga marufuku matumizi ya maji taka kutoka katika mabwawa hayo na  wameongeza walinzi wa suma JKT kwa ajili ya ulinzi zaidi.

Hata hivyo amebainisha kuwa kuna mabwawa manne ya maji taka katika eneo la swaswa ambayo ndiyo wananchi wanayatumia katika kilimo.



Febuary Mwaka huu Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Kangi Lugola aliiagiza Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dodoma (DUWASA) kutoa elimu kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya mabwawa yanayohifadhi maji taka kutoyatumia maji hayo kwa kilimo au matumizi yoyote ya nyumbani.

Lugola alitoa agizo hilo mjini Dodoma alipofanya ziara katika mabwawa yanayohifadhi maji taka yaliyopo maeneo ya Swaswa, ambapo wananchi wa maeneo hayo wameonekana wakiyatumia maji hayo katika kilimo na wengine kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya nyumbani.


Na,Mindi Joseph                                                                 Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...