Skip to main content

WALIMU ZAIDI YA ELFU TATU WALIONDOLEWA KAZINI KUPISHA UHAKIKI

            Image result for NAIBU WAZIRI KAKUNDA







Serikali imesema jumla ya walimu 3655 waliondolewa kazini baada ya kubainika kuwa na vyeti bandia kufuatia zoezi la uhakiki wa vyeti lililofanywa na serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17 hadi 2017/18.

Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za mitaa TAMISEMI Mh. Joseph Kakunda ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma katika mkutano wa Bunge alipokuwa akijibu swali la Mbunge Nassoro Seleman aliehoji ni wafanyakazi wangapi waliopoteza ajira zao katika sekta ya elimu kufuatia zoezi hilo.

Naibu Waziri Kakunda amesema katika zoezi la uhakiki wa vyeti feki Serikali ilidhamiria kubaini watumishi wa umma walio kuwa na vyeti halali na vyeti vya kugushi zeozi lililofanikisha kubaini idadi ya walimu 3655 waliokuwa na vyeti vya kugushi.

Amesema baada ya zoezi hilo yalijitokeza malalamiko pamoja na rufaa mbalimbali kwa watumishi waliodhani wameonewa na baada ya Serikali kufanya uchambuzi wa kina iliwarejesha kazini watumishi wapatao 1907 walioondolewa kazini kimakosa huku akiweka wazi hakuna kiinua mgongo chochote kitakacho tolewa na Serikali kwa watumishi walio ondolewa kazini  wakati muda wao wa kustaafu ukiwa umekaribia.

Ikiumbukwe kuwa April 28 mwaka 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli akipokea ripoti ya uhakiki wa vyeti feki katika ukumbi wa Chimwaga hapa Jijini Dodoma aliagiza kuondolewa kazini watumishi zaidi ya 19706 waliobanika kugushi vyeti ili kujipatia ajira.

Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma liliendeshwa na serikali kuanzia mwezi october mwaka 2016.

Na Pius Jayunga                                                Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...