Skip to main content

WAKULIMA WASHAURIWA KUTUMIA DAWA KWENYE MAZAO KUEPUKA VIWAVI JESHI


Image result for WADUDU WA VIWAVI JESHI





Wananchi Mkoani Dodoma wametakiwa kununua dawa kwa ajili ya kuuwa wadudu vamizi wanaoshambulia mimea katika maduka yanayotambulika  na zilizoshahuriwa na wataalamu wa kilimo ili kuepuka kununua dawa zisizokuwa na ubora na kusababisha hasarara katika mimea.

Ushauri huo umekuja baada ya kuibukua kwa mlipuko wa mdudu anayejulikana kwa jina la viwaji jeshi anayeshambulia mimea hasa ya mahindi katika mashamba.

Akizungumza na Dodoma FM Afisa Kilimo wa Mkoa wa Dodoma Bw. Bernad Abraham amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya wakulima kununua dawa zilizokwisha muda wake na zilizopoteza ubora na kushindwa kufanya kazi wakati wa kuipeleka shambani kwa ajili ya matumizi.

Bw. Bernad amesema kila wanapopata taarifa ya kuwepo kwa wadudu hao wanachukua jitihada ya kutoa elimu kwa wakulima  ili kuweza kudhibiti wadudu hao kwa njia mbalimbali wanazoelekezwa na wataalam wa kilimo .

Akizungumzia athari zilizopatikana Bw. Abraham amesema hazijaripotiwa athari kubwa kwa Mkoa wa Dodoma lakini yapo maeneo yalioathirika ikiwemo maeneo ya Dodoma Mjini pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na tayari mafunzo yamekwishatolewa kwa wakulima wa maeneo hayo.

Na Phina Nimrod                                                              DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...