Skip to main content

WAFANYABIASHARA WALALAMIKIA KITENDO CHA KUHAMISHWA MARA KWA MARA

Image result for SOKO KUU MAJENGO DODOMA





Wafanyabiashara wa soko la Sabasaba jijini Dodoma wameulalamikia uongozi wa soko hilo kuwahamisha mara kwa mara na kuwapeleka katika eneo ambalo sio rafiki kwa kufanyia biashara.

Wametoa malalamiko hayo mapema hii leo wakati wakizungumza na Dodoma FM kupitia kipindi cha Taswira ya habari ambapo wamedai kuwa uongozi wa soko hilo umekuwa na tabia ya kuwahamisha mara kwa mara na kuwapeleka mahali ambako hakuna miundo mbinu rafiki hali inayowalazimu kufanya biashara  katika milango ya maduka ya wafanyabiashara wa nguo na kusababisha ugomvi baina yao.

Akijibu malalamiko hayo mwenyekiti wa soko hilo Bwana Athumani Makole amekanusha suala la  wafanyabiashara hao kuhamishwa katika eneo lao ambapo amedai kuwa baadhi yao wamekuwa wakifanya hivyo wao wenyewe na ndipo  uongozi unapowataka kurudi katika maeneo yao huku wao wadai kuwa wanafukuzwa.

Katika hatua nyingine Taswira ya habari imezungumza na mwenyekiti wa Soko kuu  Majengo, jijini Dodoma Bwana Godson Lugazama ambapo ameuomba Uongozi wa Jiji kukarabati miundombinu ya soko hilo iliyo chakavu pamoja na kuongeza ukubwa wa soko kutokana na ongezeko la watu mbalimbali wanaoendelea kuingia mkoani hapa.

Lugazama amebainisha kuwa miundombinu hiyo imechakaa hususani mapaa na hivyo wakati wa kipindi cha masika mapaa huvuja jambo ambalo  ni kero kwa wafanyabiashara wa soko hilo.
  
Soko kuu la Majengo limejengwa tangu mwaka 1996 na linadiawa kuwa na Zaidi ya wafanyabiashara 400 wanaolipa ushuru.

Na Alfred Bulahya                                                         DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...