Skip to main content

WADAU WAISHAURI SERIKALI KATIKA KUELEKEA MAADHIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI

Serikali imeombwa kutoa ushirikiano kwa vyombo vya habari nchini ili kuendelea kutokomeza vitendo viovu katika maeneo mbalimbali ambavyo vimekuwa vikichangia kukwamisha maendeleo ya Taifa.


Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Makamu wa Rais wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bi Jane Mihanji wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya siku ya vyombo vya habari ambayo yanatarajiwa kufanyika kitaifa Mei 2 na Mei 3 mkoani hapa.

Amesema kuwa kumekuwepo na baadhi ya viongozi mbalimbali ambao wamekuwa wakijenga chuki kwa waandishi wa habari kutokana na waandishi hao kuandika habari zinazofichua maovu yanayofanywa na viongozi hao jambo ambalo linakwamisha maendeleo ya taifa ikiwemo kuwanyima haki wananchi kupata habari.

Katika hatua nyingine Bi Mahinji amewaomba wamiliki wa vyombo vya habari nchini kuhakikisha wanazingatia utoaji wa ajira kwa mikataba na kuboresha masilahi ya wafanyakazi wao kwani waandhishi wa habari wamekua wakifanya kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuisukuma serikali kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu.

Kwa upande wake mratibu kutoka Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Bwana Neville Meena amesema kuwa jukumu la kupata habari sio la waandishi wa habari pekee bali hata wananchi wana haki ya kudai taarifa kwa kiongozi yeyote  hivyo ni vyema jamii ikatambua jambo hilo ili kuunga mkono jitihada zinazofanywa na waandishi wa habari.

Bi Raziah Mwawanga ambaye ni wakfu wa vyombo vya habari amesema kuwa umefika wakati sasa wa waandishi wa habari kutumia vizuri kalamu zao kwa kuandika habari bila kumuonea mtu yeyote ili kupunguza changamoto zinazoikumba tasnia hiyo.

Siku ya uhuru wa vyombo vya habari huadhimishwa kila mwaka ifikapo may 2 na kwa mwaka huu yataadhimishwa jijini Dodoma yakiwa na kauli mbiu isemayo wajibu wa serikali , vyombo vya habari, haki na utawala wa sheria.

Na Alfred Bulahya.                                                                     Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...