Skip to main content

WADAU WA HABARI NCHINI WATOA YA MOYONI WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE KUTOKUFANYA VIZURI

                       Image result for Eda Sanga



Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na changamoto za unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwa waandishi wa habari wanawake hali inayopelekea kutokuwepo kwa wanawake wengi wanaofanya vizuri kwenye tasnia ya habari.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Bi, Edda Sanga wakati akizungumza na dodoma Fm katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari yaliyofanyika mjini Dodoma.

Bi Eda Sanga amesema kumekuwepo na baadhi ya viongozi na wamiliki wa vyombo vya habari ambao wamekuwa wakitumia nafasi zao kwakuwataka kimahusiano watumishi wao kitendo ambacho kinawadidimiza wanawake na kuwafanya wasifanye vizuri kwenye tasnia ya habari.

Amesema ukatili wa kijinsia ikiwemo unyanyasaji katika tasnia ya habari vinaumiza wanawake huku akiomba mambo hayo yasiendelee ili wanawake waweze kukua kwenye tasnia ya habari.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Usuluhishi kutoka TAMWA Bi Gladness Munuo amesema tafiti zinaonyesha kuwa  sauti za wanawake na vyanzo vya habari za wanawake bado viko chini ikiwa ni pamoja na kutokuwepo kwa wanawake wamiliki wa vyombo vya habari nchini.

Hata hivyo  Katibu wa Jukwaa La Wahariri Tanzania TEF Bwana Nevile Meena amewataka wanawake waliopo katika tasnia ya habari kupendana na kupeana ushirikiano pale wanawake wenzao wanapofanya vizuri ama kutaka msaada kutoka kwao huku akitolea mifano kadhaa kwa wanawake ambao wamekuwa wakikwamisha juhudi za mafanikio ya wanawake wenzao.

PHINNA NIMRODI                                                        Dodoma FM


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...