Waziri
mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kasimu Majaliwa amesema viwango vya
maambukizi ya virusi vya ukimwi Nchini bado ni vikubwa kwa mjibu wa utafiti wa
nne uliofanyika katika ngazi ya kaya kwa mwaka 2016 hadi mwaka 2017.
Mh.
Kasimu Majaliwa ameyasema hayo leo Jijini Dar Es Salaam wakati akizindua mkakati
wa maadhimisho ya miaka 15 tangu kuanzishwa kwa mfuko wa dharula wa Rais wa Marekani
wa kupambana na kudhibiti maambukizi ya virusi vya ukimwi (PEF)
Amesema
watu takribani Mil. 1.4 wanakadiriwa kuishi na virusi vya ukimwi Nchini wengine
themanini na moja elfu hupata maambukizi mapya ya virusi vya ukwimi kila mwaka
sawa na watu 222,000 kila siku na wahanga wakubwa wa janga hilo wakiwa ni
wasichana.
Waziri
mkuu ameitaja Mikoa inayoongoza kwa kiwango cha maambukizi
makubwa juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia 4.7 kuwa mikoa hiyo ni njombe 11.4%,
Iringa 11.3%, Mbeya 9.3% Mwanza 7.2% Kagera 6.5% Katavi 5.9%. Shinyanga 5.9% na
Dodoma ikiwa 5.0%
Ameitaja
Mikoa yenye ongezeko kubwa la watu wanaoishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi
kuwa ni pamoja na Mkoa wa Mwanza, Tanga, Kagera, Dodoma, Manyara pamoja na Mkoa
wa Iringa na kueleza kuwa takwimu hizo zinalenga kuongeza nguvu zaidi katika
kupambana na maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Ugonjwa
wa ukimwi uligunduliwa Nchini Tanzania mnamo mwaka 1983 na tangu kipindi hicho
nguvu kazi kubwa ya Taifa iliendelea kuangamia na kuchangia kupungua kwa kasi
ya utoaji wa huduma katika maeneo mbalimbali ikiwemo elimu, afya, kilimo,
ufugaji viwanda pamoja na sekta zingine.
Na Pius Jayunga
Dodoma
FM
Comments
Post a Comment