Skip to main content

VIWANGO VYA MAAMBUKIZI YA UKIMWI TANZANIA NI VIKUBWA


Image result for WAZIRI MKUU





Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kasimu Majaliwa amesema viwango vya maambukizi ya virusi vya ukimwi Nchini bado ni vikubwa kwa mjibu wa utafiti wa nne uliofanyika katika ngazi ya kaya kwa mwaka 2016 hadi mwaka 2017.

Mh. Kasimu Majaliwa ameyasema hayo leo Jijini Dar Es Salaam wakati akizindua mkakati wa maadhimisho ya miaka 15 tangu kuanzishwa kwa mfuko wa dharula wa Rais wa Marekani wa kupambana na kudhibiti maambukizi ya virusi vya ukimwi (PEF)

Amesema watu takribani Mil. 1.4 wanakadiriwa kuishi na virusi vya ukimwi Nchini wengine themanini na moja elfu hupata maambukizi mapya ya virusi vya ukwimi kila mwaka sawa na watu 222,000 kila siku na wahanga wakubwa wa janga hilo wakiwa ni wasichana.

Waziri mkuu ameitaja Mikoa inayoongoza kwa kiwango cha maambukizi makubwa juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia 4.7 kuwa mikoa hiyo ni njombe 11.4%, Iringa 11.3%, Mbeya 9.3% Mwanza 7.2% Kagera 6.5% Katavi 5.9%. Shinyanga 5.9% na Dodoma ikiwa 5.0%

Ameitaja Mikoa yenye ongezeko kubwa la watu wanaoishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi kuwa ni pamoja na Mkoa wa Mwanza, Tanga, Kagera, Dodoma, Manyara pamoja na Mkoa wa Iringa na kueleza kuwa takwimu hizo zinalenga kuongeza nguvu zaidi katika kupambana na maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Ugonjwa wa ukimwi uligunduliwa Nchini Tanzania mnamo mwaka 1983 na tangu kipindi hicho nguvu kazi kubwa ya Taifa iliendelea kuangamia na kuchangia kupungua kwa kasi ya utoaji wa huduma katika maeneo mbalimbali ikiwemo elimu, afya, kilimo, ufugaji viwanda pamoja na sekta zingine.

Na Pius Jayunga                                                                                  Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

YANGA KESHO KUJUA ANACHEZA NA NANI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

MAJINA ya vigogo wa soka Afrika, wakiwemo mabingwa wa Afrika 1998, Raja Casablanca yametawala katika orodha ya wapinzani wapya wa Yanga kwenye michuano ya Afrika. Yanga SC imeangukia kwenye kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, ambako watamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo. Hiyo ni baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Township Rollers Jumamosi jioni Uwanja wa Taifa mjini Gaborone nchini Botswana. Matokeo hayo yanamaanisha Rollers inakwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza historia hiyo kwa ushindi wa jumla wa 2-1 uliotokana na matokeo ya mchezo wa                              kwanza Dar es Salaam Machi 6. Na Yanga SC itamenyana na moja ya timu zilizofuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo, ambazo ni CR Belouizdad, USM Alger za Algeria, Al-Masry ya Misri, Djoliba ya Mali, Raja Casablanca, Enyimba ya Nigeria, SuperSport United ya Afrika K

SERIKALI IMEANZA KUANDAA KITINI CHA MASUALA YA JINSIA

                                             Serikali imeanza mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza katika kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto umekithiri sana nchini   hivyo Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo. Amesema   lengo la kuandaa kitini cha kufundishia masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii. Bi. Mboni amefafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Is