Skip to main content

UPUNGUFU WA WALIMU WA HISABABTI WASHUSHA UFAULU WA SOMO HILO

             Image result for UPUNGUFU WALIMU WA HESABU




Upungufu wa walimu wa somo la hisabati katika shule za sekondari umechangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi kutofanya vizuri  somo hilo huku wengi wao wakiacha kabisa kulisoma  na kujikita zaidi katika masomo ya sanaa.

Wakizungumza na kituo hiki baadhi ya wanafunzi wamekiri kuwepo kwa walimu wachache wa somo hilo pamoja na walimu  kuwa wakali kitu ambacho kinapelekea wengi wao kushindwa kabisa kusoma somo hilo huku pia wakikatishwa tamaa na wanafunzi waliowatangulia kwa kusema somo hilo ni ngumu.

Mwalimu SOPHIA MDEI ambaye ni mwalimu wa somo la hisabati amesema changamoto kubwa inayowakabili ni kuwepo kwa walimu wachache hali ambayo imepelekea kuwa na vipindi vingi na kusababisha kushindwa kumfuatilia mwanafunzi mmoja mmoja.

Aidha kwa upande wake afisa elimu sekondari Halimashauri ya jiji la Dodoma Mwalimu ABDALLAH MEMBE amesema kutokana na changamoto hiyo serikali tayari imeweka mkakati wa kuhakikisha somo hilo linafanya vizuri katika shule zote nchini ikiwa ni  kuongeza walimu  kwa lengo la kuimarisha ufaulu wa somo hilo.

Mwalimu MEMBE ameongeza kuwa Ili kuberesha ufaulu wa somo hilo wanafunzi wametakiwa kuacha kukata tamaa kwa kusema somo hilo ni gumu badala yake kuweka jitihada nyingi kama wanavyofanya katika masomo mengine.

Na,Mindi Joseph                                                             Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...