Skip to main content

UNESCO YAENDESHA WARSHA YA KUPINGA UKEKETAJI KWA KUSHIRIKISHA REDIO ZA JAMII

Image result for WARSHA YA KUPINGA UKEKETAJI LOLIONDO






Wadau wa kupinga vitendo vya ukeketaji wametoa maoni yao kwa kuitaka serikali kuanzisha mitaala ya somo la kupinga ukeketaji kuanzia shule za msingi na sekondari Nchini. 

Wametoa maoni Hayo wakati wa warsha ya kupinga vitendo vya ukeketaji inayoendelea katika tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro mkoani Arusha. 

Akizungumza na Dodoma Fm Mwenyekiti wa Malaigwanani Bwana Joseph Tripai wakati akiwasilisha Mada juu ya kutokomeza vitendo vya ukeketaji ameitaka serikali kupitia Wizara ya elimu kuanzisha mtaala wa somo hilo ili kuanza kutoa elimu y'a kupinga vitendo hivyo kuanzia kwa watoto wa shule wangali wadogo.

Kwa upande wake Afisa wa polisi wa dawati la jinsia Wilayani Ngorongoro Remmiguis Williams amebainisha Changamoto kadhaa ikiwemo usiri kutoka kwa wazazi, ndugu Na jamii kwa ujumla zimekua zikirudisha nyuma jitihada za kutokomeza vitendo vya ukeketaji.

Ameongeza kuwa baadhi wanajua vitendo vya ukeketaji ni kosa kisheria  hivyo huogopa kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa kuhofia ndugu zao kupelekwa mahakamani na kufungwa.

Warsha hii inaendelea wilayani Ngorongoro katika tarafa ya Loliondo kwa kushirikiana Na shirika la Umoja wa Mataifa elimu sayansi Na utamaduni UNESCO ambapo imewakutanisha baadhi ya Waandishi kutoka katika Mikoa mitano inayoongoza kwa vitendo vya ukeketaji ikiwemo, Manyara, Dodoma, Mara, Arusha na Singida. 

Na Lucas Godwin                                            Chanzo:Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...