Skip to main content

UHARIBIFU HUU NDIO CHANZO CHA MKOA WA DODOMA KUPOTEZA MAHINDI MENGI


Image result for MAHINDI YANAHARIBIWA NA WADUDU DODOMA





Kutokana na  Athari za mabadiliko ya tabia nchi katika mfumo wa  Ki-ekolojia na Usalama wa Chakula Mashariki mwa Afrika, jamii imetakiwa kuchukua hatua thabiti kukabiliana na mabadiliko hayo.


Mkoa wa Dodoma unatajwa kupoteza mahindi ambayo inagharimu  kiasi kikubwa cha fedha kila mwaka kutokana na wadudu  waharibifu.

Hayo yamebainisha  katika Kata ya Hombolo Bwawani Jijini Dodoma na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Kilimo ukanda wa Kitropiki (IITA) wakati wa kutoa elimu kuhusu kilimo kwa kutumia shamba darasa.

Kwa mujibu wa muwakilishi wa shirika hilo  Dk. Fredy   amesema kuwa, elimu hiyo ya shamba darasa kwa wakulima ni kipimo kwa Utafiti  wa wadudu wanaoharibu mazao na unalenga katika kupata suluhu ya kukabiliana na magonjwa ya mahindi, akiwemo funza ambaye amekuwa ni mharibifu  katika zao la mahindi,  katika ukanda wa kati.

Pamoja na hayo mtaalamu huyo amesema kuwa IITA imejipanga kuwajengea uwezo wakulima hao kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia tekinolojia muhimu katika ikiwemo kuanzisha mashamba yanayoonyesha kilimo cha kukabiliana na mabadiliko hayo.

Kutokana na hayo mhifadhi wa udongo na uvunaji wa maji ya mvua shambani kutoka taasisi ya utafiti Hombolo Bw.Elirehema Swai aliishauri taasisi ya IITA kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa wakulima nchini kuhusu kadhia ya Sumu Kuvu kwa mazao ya chakula.

Kwa upande wake muwakilishi wa katibu mkuu wizara ya kilimo Bi.Shakwanende Natai aliwataka wakulima wa kata ya Hombolo kutumia mbegu bora ili kuepusha magonjwa kwa mimea kwa kuzingatia utaalamu wa kisasa.

Naye Afisa kilimo wa Halmashauri wa jiji  George Mhina aliwaambia wakulima wa kata ya Hombolo kuchukua jukumu la kukagua mazao mara kwa mara na pindi wanapoona mabadiliko yasiyo ya kawaida watoe taarifa mapema kwa wataalamu wa kilimo .

Mbali na hayo amesema,ili wakulima hao wapate mazao yanayostahili wanapaswa kuzalisha kisasa kwa kuwatumia wataalam wa kilimo ikiwa ni pamoja na kuzingatia mazao yanayostahili ukame.

Na ANIPHA RAMADHAN                                  CHANZO:DODOMA FM






Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...