Skip to main content

TARATIBU ZA KISHERIA ZA KULITAMBUA RASMI JIJI LA DODOMA ZAANZA KUFANYIKA

              Image result for WAZIRI Mkuu



Kufuatia tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kuitangaza Dodoma kuwa Jiji, Waziri mkuu Kasimu Majaliwa amesema tayari taratibu za kulitambua Jiji la Dodoma kisheria zimeshaanza kufanyika.

Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa kuteuliwa Felista Aloyce Bula aliehoji ni lini Serikali italeta mswada wa sheria wa kuitambua Dodoma kama Jiji.

Amesema kama ambavyo Mh. Rais ana mamlaka ya kutangaza eneo lolote kulipa hadhi ya Jji, hivyo Serikali kupitia vyombo vyake huanza taratibu za kuingiza maelekezo hayo kisheria na tayari wanasheria, Tamisem, ofisi ya Waziri mkuu wameanza kufanyia kazi swala hilo ili litambulike rasmi kisheria.

Waziri mkuu amesema kisheria Rais ana mamlaka ya kupandisha hadhi mji wowote iwapo umekidhi vigezo muhimu ikiwemo huduma ya maji, afya, miundombinu ya barabara sambamba na kuimarika kwa zoezi la ukusanyaji wa mapato vigezo ambavyo Jiji la Dodoma limekidhi.

Waziri Mkuu amewataka wakazi wa Dodoma kutumia fursa hiyo kama sehemu ya wao kujiongezea kipato kupitia shughuli mbalimbali kutokana na Dodoma kukua ikienda sambamba na ongezeko la mahitaji muhimu ikiwemo chakula kwa wakazi wa Jiji la Dodoma.

Na Pius Jayunga                                                      Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...