Skip to main content

SUMATRA YASISITIZA MARUFUKU BODABODA KUBEBA WATOTO CHINI YA MIAKA 9.

           Image result for MARUFUKU BODABODA KUPAKIA WATOTO CHINI YA MIAKA 9




Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) jijini  Dodoma kwa kushirikiana na jeshi  la polisi imetoa tahadhari kwa waendasha bodaboda kutobeba  watoto wenye  umri chini ya miaka 9.

Akizungumza na DODOMA FM mapema leo Afisa mfawidhi wa SUMATRA Bwana Konradi Shio amesema sheria hairuhusu kubeba mtoto peke yake kwenye pikipiki za magurudumu mawili licha ya kuwepo kwa madai ya bodaboda kuwa wanajipatia kipato.

Bwana Shio ameongeza kuwa kwa mujibu wa sheria wanawachukulia hatua kali bodaboda kwa kuwatoza faini, na kuwapeleka jela lakini bado kuna upuuzwaji wa sheria hiyo hivyo wamekuwa wakipendekeza kuwapeleka mahakamani ili kupewa fundisho.

Katika Hatua nyingine amebainisha madhara ya kubeba mtoto chini ya umri wa miaka 9 kwenye bodaboda na tayari wameanzisha operationi ambayo inafanywa na jeshi la polisi muda wa asubuhi watoto wanapoenda shule pamoja na jioni wanaporudi kutoka shule ili kuhakikisha  bodaboda hao wanawakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

Ili kuondokana na changamoto hii  waendesha bodaboda wametakiwa kuacha kuwabeba watoto hao chini ya umri wa miaka 9  ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria za barabarani.

Na,Mindi Joseph                                                              Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...