Skip to main content

SPIKA WA BUNGE ANATAMBUA MCHANGO WA WANAHABARI KATIKA MAENDELEO YA NCHI



 


Imeelezwa kuwa wanahabari wana jukumu la kuhakikisha wanaijenga jamii na kuifanya huwa imara kwa kuwafikishia taarifa za usahihi pamoja na kufichua matukio ya uhalifu ikiwemo  dawa za kulevya.

Hayo yameelezwa na Spika wa bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai katika kongamano la maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani ambayo kitaifa yamefanyika hapa Jijini Dodoma.

Spika Ndugai amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya baadhi ya watu kusambaza matukio ya uongo katika Mitandao mbalimbali ya kijamii hali inayopelekea usumbufu na sintofahamu kwa jamii.

Nae Makamu wa Rais wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania Bi.Jane Mihanje amesema katika kuhakikisha wanahabari wanatumia kalamu na karatasi kwa ajili ya maslahi ya wananchi wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali ikiwemo  baadhi ya wanahabari kukutana na matukio ya kutekwa pamoja na kuuawa.

Aidha Bi Jane amesema kuwa wanahabari wanahofia kufanya kazi kwa Uhuru kutokana na vitisho wanavyokutana navyo hivyo Serikali ikemee na kuvipinga vitendo hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mashindano ya Ulimbwende nchini Tanzania Bi. Salome Kitari ameiomba Serikali kukemea matukio yanayofanywa juu ya wanahabari hususani ya kutekwa .

Maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo Vya Habari Mwaka 2018 yamebebwa na Kauli Mbiu isemayo wajibu wa sheria, vyombo vya habari, haki na sheria.

Na Phinna Nimrodi                                                                 Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...